Waamini wajitolea kujenga Kanisa Tabora



KASI ya ujenzi wa Kanisa la Parokia ya Familia Takatifu Ipuli Jimbo Kuu Katoliki Tabora unaendelea kwa kasi huku waamini wa parokia hiyo wakitarajia kuukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.
Akizungumza na Gazeti hili Paroko wa Parokia hiyo Padri Ponsiano Kibobera amesema wamefikia uamuzi wa kujenga Kanisa hilo yakiwa ni matokeo ya ongezeko la kasi la idadi ya waamini hali iliyosababisha Kanisa la zamani kutokabiliana na ongezeko hilo.
Padri Kibobera ameliambia Gazeti hili kuwa Kanisa linaloendelea kujengwa ni matunda ya kazi ya waamini wenyewe bila kupata msaada wowote toka nje hali inayoonesha ukomavu wa Imani waliyoipokea miaka mingi iliyopita.
Aidha amesema wana parokia wamejipangia kulijenga Kanisa kwa utaratibu wa jumuiya ndogondogo na vikundi mbalimbali vya vyama vya kitume.
Kanisa hilo litawapatia waamini fursa ya kujipatia eneo zuri, tulivu la wao kufika kwa ajili ya kusali, kuomba, kumsifu na kumshukuru Mungu.
Padri Kibobera amesema mpaka sasa ujenzi wa Kanisa hilo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 147, 000, 0000 za kitanzania.  Kanisa hilo lipo katika hatua  ya msingi, na hadi linakamilika litagharimu shilingi Bilioni 2 za kitanzania.
Parokia ya Familia Takatifu Ipuli ilianzishwa mwaka 1972 na kukamilika mwaka 1983 chini ya uongozi wa mapadri wa shirika la Wajezuiti waliokuwa na makao yao hapo Tabora.
Kanisa hilo likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua waamini 2500 waliokaa kwa wakati mmoja.


Comments

  1. NIMEFURAHI KULIONA KANISA HILO KIUKWELI IPULI IMEKUWA KWA KASI SANA NA KANISA TULILOKUWA TUKITUMIA LILIKUWA DOGO, NA HAPO TULISHAHAMA KUTOKA MISUFINI AMBAPO NDIO KANISA LA PAROKIA LILIPOKUWA AWALI NA NDIO KANISA LANGU NILILOBATIZIWA , KANISA AMBALO LINAENDELEA KUTUMIKA NALO NILIWEZA KUPATIA SAKRAMENTI YA KIPAIMARA NAWAPONGEZA WANA FAMILIA WOTE YA IPULI KWA KAZI KUBWA MLIYOIFANYA MUNGU AWAONGEZEE MLIPO PUNGUZA. NAITWA JULIUS LUSWAGA WA KIGANGO CHA MAGEREZA PAROKIA YA IPULI KWA SASA NIPO PAROKIA YA WATAKATIFU WOTE NZUGUNI JIJINI DODOMA

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU