MARA WATAKIWA KUSHIRIKI KWA WINGI WIKI YA MAZINGIRA KITAIFA





MKUU wa Mkoa wa Mara Dk Charles Mlingwa amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya siku ya mazingira yanayofanyika Kitaifa Mkoani humo katika uwanja  wa Mwenge wilayani Butiama kuanzia Juni 1-4 mwaka huu.

Akizungumza na wandishi wa habari katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika ofisi ya mkuu wa Mkoa, mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa maadhimisho ya siku ya mazingira kitaifa yalitarajiwa yatazinduliwa rasmi na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.January Makamba Juni mosi mwaka huu wilayani Butiama.

Mlingwa amefafanua kuwa baada ya uzinduzi huo kutakuwepo na Kongamano na tafrija  mbalimbali kuhusiana na masuala ya mazingira kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoka nje na ndani ya Mkoa watakaowasilisha mada mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na athari za uharibifu wa mazingira, ambapo jumla ya miche 1500 itapandwa wakati wa maadhimisho hayo katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Butiama.

Amezitaja baadhi ya mada zitakazotolewa kuwa ni pamoja na kuelimisha wananchi kupanda miti ili kuhifadhi mazingira na kukidhi mahitaji ya dunia katika kupambana na ongezeko la  hewa ukaa, kuijengea jamii uwezo juu ya uelewa wa masuala ya mazingira na changamoto za kijamii zinazijitokeza katika kutunza mazingira, kwa kuwa Mkoa wa Mara ni miongoni mwa mikoa ambayo ina uharibifu mkubwa wa mazingira .

Amesema lengo kubwa la kufanya maadhimisho hayo ya Kitaifa wilayani Butiama ni kuenzi kazi zote za uhifadhi wa mazingira zilizofanywa na Baba wa Taifa  Mwalimu  Julius K. Nyerere katika kuhifadhi mazingira enzi za uhai wake .

Neema Chausiku, mkazi wa mjini Musoma amesema kuwa mkoa wa Mara ni moja kati ya mikoa inayotumia nishati ya mkaa na kuni kwa wingi, hivyo maadhimisho hayo yatawasaidia wananchi kupata elimu kuhusiana na upandaji wa miti na uhifadhi wa mazingira kwa ujumla, ili kuepukana na ukame ambao wamekuwa wakikabiliana nao.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufungwa rasmi Juni 4 mwaka huu na makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU