Posts

Showing posts from September, 2018

Msimamo wa Magufuli kuhusu uzazi wa mpango wapongezwa

Image
Na Pascal Mwanache, Dar M SIMAMO alioutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli juu ya uzazi wa mpango umepongezwa kwa kuwa kukithiri kwa vitendo vya matumizi ya vidhibiti mimba kumeharibu taifa na kushambulia maadili, utamaduni na imani ya taifa huku dhana hizo zikiwa ni itikadi ovu za magharibi za kudhibiti ukuaji wa idadi ya watu. Pongezi hizo zimetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea Uhai nchini (Pro life) Emil Hagamu katika tathmini yake ambapo amesema kuwa watu wa Ulaya wamepita katika miongo mbalimbali, imefikia mahali wameharibikiwa hivyo mawazo na itikadi zao ovu ndizo zinazoletwa kwetu Afrika hasa Tanzania. “Hiki ndicho Nyerere alichosema, alisema ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Kwa hiyo watu ndiyo namba moja. Asikudanganye mtu, nchi zote za Ulaya zilipata maendeleo kwa sababu kuu tatu: Walitunyonya kiuchumi na kisiasa, biashara ya utumwa ambapo walihitaji watu, na idadi yao ni kubwa. Uki promote co

Niko tayari kuwatumikia -Ask. Ruwaich

Image
+ Kard. Pengo aeleza sababu za kuomba mwandamizi  Na Na Pascal Mwanache, Dar es salaam A SKOFU Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Yuda Thadei Ruwaich amesema kuwa amepokea kwa shukrani uteuzi wake na kuwaeleza waamini wa jimbo hilo kuwa yuko tayari kuwatumikia kwa utii licha ya changamoto za mazingira mapya ambazo huenda atakutana nazo. Ameeleza hayo katika Misa Takatifu ya kupokelewa kwake jimboni Dar es salaam, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Septemba 7, 2018 na kuhudhuriwa na mamia ya waamini wa jimbo hilo. “Napokea yote kwa shukrani nikijiaminisha mikononi mwa Mungu. Ninayo nia thabiti ya kushirikiana nanyi katika kulihudumia taifa la Mungu, kwani katika Kanisa huwa hakuna kuhama; kuna kutumwa na kutumikia. Niko tayari kuwatumikia” ameeleza Askofu Ruwaich. Aidha Askofu Ruwaich ameahidi kuwaombea wana Jimbo Kuu Katoliki Mwanza wanapoingia katika kipindi kipya cha kuwa katika jimbo lisilokuwa na mchungaji m

Sherehe za miaka 80 ya utume wa Chama cha Kitume cha Legio Maria hapa nchini na miaka 97 kiulimwengu. Maadhimisho hayo yamefanyika katika Parokia ya Kristo Mfalme Tabata Jijini Dar es Salaam

Image