Posts

Showing posts from July, 2017

MAGAZETINI LEO JUMATATU JULAI 31

Image

MWITO: WAZAZI NA WALEZI WAWARITHISHE WATOTO UTU MWEMA

Image
Parokia ya Mtakatifu Anna, iliyoko ndani ya Vatican, Jumatano, tarehe 26 Julai 2017 imeadhimisha kumbu kumbu ya Watakatifu Yoakim na Anna, wazazi wake Bikira Maria kwa kusali kwa ajili ya kuombea maadhimisho ya Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya vijana, yatakayotimua vumbi kuanzia mwezi Oktoba, 2018 hapa mjini Vatican kwa kuongozwa na kauli mbiu “Vijana, Imani na Mang’amuzi ya Miito”. Waamini wamesali pia kwa ajili ya kuombea maadhimisho ya Siku ya XXXIV ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2019 yatakayoadhimishwa nchini Panama kuanzia tarehe 22- 27 Januari 2019 kwa kuongozwa na kauli mbiu “Tazama mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema”. Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu, ameongoza Ibada ya Misa Takatifu Parokiani hapo majira ya jioni! Wakati wa Ibada ya Misa ya Asubuhi, Kardinali Angelo Comastri, Mwakilishi wa Baba Mtakatifu kwa mji wa Vatican, katika mahubiri yake alikazia umuhimu wa wazazi kutekeleza dhamana na wajibu wao wa m

KUELEKEA MIAKA 100 YA UPADRI: KILOMBERO WAPATA PADRI WA KWANZA MJESUITI

Image
Na Tuzo Nyoni, Ifakara Wakati maandalizi ya maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 100 ya Upadri nchini yatakayofanyika katika Jimbo Kuu Katoliki Dodoma yakiendelea vizuri, wito kwa mapadri nchini umeendelea kutolewa kuwa wazingatie kuwa wametumwa kwa watu ili wawasaidie kuondokana na matatizo mbalimbali na hatimaye wajisikie kuwa wao pia ni wana wa Mungu. Akihubiri katika adhimisho la misa takatifu ya shukrani ya Padri Patrick Ngamesha(PICHANI) iliyofanyika hivi karibuni katika Kanisa la Mtakatifu Siliakus parokiani Mang’ula   Jimbo Katoliki Ifakara, Padri Valelian Shirima aliyewahi kuwa Mkuu wa Shirika la Majesuiti   amesema kuwa Kanisa lote la Mungu lina haki ya   kusherehekea sikukuu hiyo kwa ajili ya makuu aliyoyatenda kupitia nafsi ya padri mpya Patrick Ngamesha. Padri Shirima amesema mapadri wamepewa mamlaka ya kuwasafisha watu dhambi zao na wanapokutana na watu wenye mioyo migumu wasichoke kuwahubiria neno la Mungu, kazi ambayo mapadri wanaifanya katika maisha yao y

MIAKA 75 YA UTUME: SI MCHEZO

Image
Na Thomas Mambo, Tabora HUKU Kanisa Katoliki Tanzania likiadhimisha Jubilei ya Miaka 100 ya Upadri, waamini nchini wamekumbushwa wajibu wao wa kuwa na moyo wa shukrani kwa Mwenyezi Mungu kwa kuwatoa watoto wao ili waingie katika miito ya Upadri na Utawa na waweze kuisaidia jamii kudumisha upendo, amani, maelewano na maendeleo. Padri John Mungoni wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora ametoa wito huo hivi karibuni katika Misa Takatifu ya kumpongeza Sister Maria Macktilda Nyanzala aliyesherehekea miaka 75 ya utume wake katika Shirika la Mabinti wa Maria Tabora. Padri Mungoni amesema wana Itaga wanayo sababu ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya Sr. Nyanzala anayetoka katika Parokia ya Itaga na kusema waamini lazima wajitafakari na kuanza maisha mapya ya kuona kuwa Kanisa linapata miito hiyo mitakatifu na kuachana na mazoea ya kuona wito wa ndoa ni muhimu zaidi ya miito mitakatifu. Aidha padri Mungoni amesema Parokia ya Itaga pia inapaswa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa na map

UPATANISHO: KARATU WAANDAA MISA MAALUM

Image
Na Sophia Fundi, Karatu. PAROKIA ya Karatu katika Jimbo Katoliki Mbulu kwa mara ya kwanza tangu ianzishwe mwaka 1946 imeadhimisha misa ya upatanisho kwa walei na mapadri waliowahi kufanya utume katika parokia hiyo akiwemo marehemu padri John Costigan wa Shirika la wapalotini ambaye ndiye mwanzilishi wa parokia hiyo. Misa hiyo ni hitimisho la Mfungo wa Novena ya siku tisa ya kuomba Huruma ya Mungu ambapo waamini walishiriki katika Jumuiya ndogondogo za kikristo na  hatimaye kushiriki adhimisho la misa iliyohudhuriwa na mapadri zaidi ya 30, wakiwemo mapadri wote waliowahi kufanya utume katika parokia hiyo na mwakilishi wa Shirika la wapalotini ambaye ni mkuu wa Shirika hilo jimboni Mbulu, viongozi wa Serikali katika Wilaya ya Karatu, wabunge Jimbo la Karatu, viongozi wa siasa na wazee maarufu. Akihubiri katika Misa hiyo, paroko wa parokia hiyo padri Pamphili Nada amesema kuwa tukio hilo la kuadhimisha misa ya upatanisho ni zoezi lililoibuliwa na walei wa

Kardinali Pengo: Miaka 25 iliyotukuka

Image
n   Na Pascal Mwanache ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameadhimisha Jubilei ya miaka 25 ya kuliongoza Jimbo hilo, na kusema kuwa ushirikiano kati yake na waamini ndiyo uliowezesha mafanikio mbalimbali katika utume wake ikiwa ni pamoja na kuanzisha Parokia 87. Katika Misa hiyo ya shukrani iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mt. Yosefu, Kardinali Pengo amewashukuru waamini kwa sala zao kwa muda wote alipokuwa akipatiwa matibabu, na kusema kuwa kwa sasa afya yake imeimarika na ameshuhudia makuu ya Mungu. “Nilipotoka katika chumba cha upasuaji nilisema maneno haya: ‘Sitakufa bali nitaishi ili niyasimulie matendo makuu ya Mungu’. Ninawashukuru wanajimbo ambao wameifanya miaka 25 ikamalizika kwa haraka. Hii inatokana na ukweli kwamba mmoja anatoa amri na wengi wanatenda” amesema Kardinali Pengo wakati akitoa shukrani kwa waamini. Akitoa homilia katika misa hiyo Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Euseb