Posts

Showing posts from June, 2019

Huwezi kutenganisha utume wa walei na maendeleo ya Kanisa- Kard.Pengo asema

Image
IMEELEZWA kuwa waamini walei nchini wamekuwa chachu ya maendeleo ya Kanisa kwa ushiriki wao kikamilifu katika mipango na utekelezaji wake katika hatua mbalimbali. Hayo yameelezwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya jubilei ya miaka 50 ya utume wa walei Tanzania, yanayotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Msimbazi Center jijini Dar es salaam na kufikia kilele chake Juni 16, 2019. Kardinali Pengo ameeleza kuwa walei hawapaswi kujiona kuwa ni watu wa kuambiwa tu kana kwamba hawana mchango wowote, bali wanapaswa kuona kuwa wao ni sehemu muhimu ya maendeleo ya Kanisa. “Kabla ya Mtaguso Mkuu wa pili wa Vatikani waamini walei walisubiri watekelezewe kila kitu kana kwamba hawana chochote cha kutoa. Baada ya mtaguso huo Kanisa limetambua nafasi ya walei na hivyo ni lazima wajue kuwa wana sehemu muhimu ya kufanya, siyo tu kulipa zaka na kusikiliza maelekezo” ameeleza Kardi

Ask. Nyaisonga aongoza waamini Iringa kwenye Jubilei za Mapadri

Image
askofu Mkuu wa Jimbo Kuu   Katoliki Mbeya Mhashamu Gervas Nyaisonga   hivi karibuni ameongoza waamini wa Jimbo Katoliki   Iringa katika maadhimisho ya jubilei mbalimbali za mapadri wa jimbo hilo. Walioadhimisha Jubilei ni pamoja na Monsinyori Julian Kangalawe Pelate ambaye ameadhimisha miaka 50 ya Upadri. Pia walikuwemo mapadri walioadhimisha Jubilei ya miaka 25 ya upadri akiwemo Padri   Richard Chatila Paroko wa Parokia ya Kihesa,   Padri Paul Msombe Paroko wa Parokia ya Ipogolo,   Padri Baptist   Duma Paroko wa   Parokia ya Mdabulo,   Padri Christopher Nyoni mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki RUCU na Padri Cephas Mgimwa ambaye pia anafanya kazi Chuo Kikuu   cha Kikatoliki RUCU ambaye hakushiriki Misa hiyo yupo nje ya nchi kwa majukumu mengine. Akitoa homilia katika Misa hiyo ambayo imefanyika katika ukumbi wa Seminari ya malezi Mafinga na kuhudhuriwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa, Askofu wa Jimbo Katoliki Ifakara Mhashamu Salitar

Askofu Nzigilwa apongeza Utume wa Halmashauri ya Walei Tanzania

Image
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam, Mhasham Euzebius Nzigilwa ameungana na waamini na viongozi wa Halimashauri ya Walei Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam katika kuadhimisha jubilei ya dhahabu ya miaka 50 ya utume wao. Akitoa homilia yake wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya adhimisho hilo lililofanyika kwenye viwanja vya Msimbazi centre Dar es salaam, Askofu Nzigilwa amesema kuongezeka kwa imani nchini kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na uwepo wa utume wa halimashauri ya walei.   “Nia ya Askofu Mkuu wa Jimbo hili Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo ya kutaka kujengwe nyumba za mapadri kwaajili ya kuwasogezea waamini huduma za kiroho kutoka kwa mapadri ilichagizwa kwa kiasi kikubwa na uwepo wa halimashauri ya walei. Na utume wao tangu mwanzo umelipa jimbo letu nguvu ya kuinjilisha na kukua kwa imani,” amesema Askofu Nzigilwa. Aidha ametoa wito kwa Halmashauri ya Walei Jimbo na kwa waamini wote waliobatizwa kuendelea kuishi kitakatifu katika wito wowote wanaoitiwa