Posts

Showing posts from November, 2016

MAHAFALI (RUCO) PICHANI

Image
NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Simon Msanjila amewaasa wahitimu wa Chuo Kikuu Katoliki Ruaha (RUCO) kuwa mabalozi wazuri wa chuo hicho kwa kupambana na kukemea rushwa na ufisadi....maelezo zaidi SOMA KIONGOZI IJUMAA HII

MAMBO YALIVYOKUWA MAHAFALI SEKONDARI DON BOSCO JIMBO KATOLIKI SHINYANGA

Image
Askofu wa jimbo katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu ametoa wito kwa  jamii kuwekeza zaidi katika elimu kwa upendeleo wa kuwasomesha  watoto wa kike na kuacha mila na desturi mbaya ya kuwaozesha kwa tamaa ya ng’ombe...zaidi, SOMA KIONGOZI IJUMAA HII

Amoris laetitia ni kwa ajili ya huduma ya Injili ya familia!

Image
Baba Mtakatifu Francisko kupitia Wosia wake wa Kitume Amoris laetitia , yaani Furaha ya Upendo ndani ya familia , anaonesha kuheshimu na kujali changamoto ambazo familia zote wanakumbana nazo kwa namna moja au nyingine. Kardinali Lorenzo Baldisseri, katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu amesema kuwa, Wosia huo wa kitume umefika kwa wakati muafaka ambapo familia zimo kwenye kinzani kubwa kihistoria. Kinzani kutambua wajihi wake, kujitambua kijinsia mwanamke na mwanaume, kuheshimu tunu ya ndoa na familia, kutunza uhai na haki msingi za watoto na kila mwana familia, kujaliana na kupendana kwa furaha. Wosia wa kitume, Amoris laetitia , unaeleza kwamba ni ngumu kuwatia moyo wana ndoa kuhusu uaminifu na kujitoa kwa kila mmoja bila kutia cheche hija ya kukua, kukomaa na kuzama katika upendo kati ya wana ndoa na ndani ya wanafamilia wote. Kwa sababu upendo ndio chemichemi na msingi wa ndoa, na upendo huo katika kukua na kukomaa kwake unarutubika na kupanuka kwa kuzaa na kulea watoto, na kuw

Kanuni bora za mawasiliano kadiri ya Papa Francisko!

Image
Alessandro Gisotti, mwandishi wa habari wa Radio Vatican amechapisha kitabu kinachopembua kanuni kumi za mawasiliano bora mintarafu mwelekeo wa Baba Mtakatifu Francisko, kitabu ambacho kitaanza  kuuzwa kwenye maduka ya vitabu kuanzia sasa. Mawasiliano ya jamii yanapaswa kusaidia mchakato wa ujenzi wa madaraja ya watu kukutana na kusaidiana na wala si kuta zinazowatenganisha watu! Wala kinzani na migawanyiko inayodhalilisha utu, heshima na mafungamano ya kijamii. Kardinali Luis Antonio Tagle, Rais wa Shirikisho la Mashirika ya Misaada ya Kanisa Katoliki Kimataifa ndiye aliyeandika utangulizi wa kitabu hiki. Fedha yote itakayopatikana itatumika kwa ajili ya kugharimia miradi ya maendeleo endelevu inayotekelezwa na Wasalesiani wa Don Bosco. Baba Mtakatifu amekuwa ni kielelezo cha ushuhuda na chombo cha kukutana na watu katika maisha na utume wake, hata wale ambao kutokana na magonjwa na hali zao za maisha wanajikuta wametengwa na jamii, kama ilivyokuwa ugonjwa wa Ukoma kwenye Agano

Kanuni za kuzingatia kuhusiana na vitega uchumi vya watawa

Image
Kongamano la Pili la Kimataifa kuhusu uchumi, lililokuwa limeandaliwa na Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za kitume lililofunguliwa hapo tarehe 25 Novemba 2016 limefungwa rasmi, Jumapili tarehe 27 Novemba 2016 kwa kutoa mwongozo unaopaswa kufanyiwa kazi na watawa kwa siku za usoni ili kuendelea kuwa waaminifu kwa karama za Mashirika yao, huku wakiwa na mwelekeo mpana zaidi kuhusiana na masuala ya kiuchumi. Kardinali Joao Braz de Aviz, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume amewakumbusha watawa kwamba, wanapaswa kuwa makini zaidi na masuala ya kiuchumi, kwa kuhakikisha kwamba, wanatumia weledi, ujuzi, mang’amuzi na historia ya Mashirika yao, ili kuendelea kuwa ni mashuhuda wa tunu msingi za Kiinjili hata katika masuala ya kiuchumi. Lengo ni kuendelea kuwa waaminifu kwa karama za Mashirika haya, lakini kwa kusoma alama za nyakati pamoja na kuangalia changamoto zinazoendelea kujitokeza katika masuala ya uchumi na maendeleo pamoja na a