Ask. Minde: Tujitathmini na kuidhihirisha huruma

ASKOFU wa Jimbo Katoliki Kahama, Mhashamu Ludovick Minde amesema kuwa kila mkristo anapaswa kufanya tathmini ya kina baada ya kuhitimishwa kwa Yubilei  ya Huruma ya Mungu, huku akitoa angalizo Huruma ya Mungu ipo kila wakati.

Askofu Minde ameeleza hayo katika maadhimisho ya kufunga na kufungua mwaka Endelevu wa Huruma ya Mungu, Jimbo Katoliki Kahama, yaliyofanyika Novemba 19, 2016 siku moja kabla ya kufunga mwaka wa huruma ya Mungu katika Kanisa la Ulimwengu.
Amesema kuwa kitendo cha kufungua mlango wa Kanisa Kuu kama ishara ya kufungua rasmi mwaka wa huruma ya Mungu ni tendo la nje. Tendo hili linawaalika waamini wafungue mioyo yao na maisha yao ili kujitakasa na kujisafisha.

Hiki ni kipindi cha toba, tutoe nafasi, tujisafishe, tujitakase,tuwe donge jipya kwa Mungu aweze kumwaga huruma yake kwetu” ameeleza.

Aidha Askofu Minde ametoa rai kwa waamini kuwa tayari kutoa huruma kwa wengine.

 “Tunapopokea huruma ya Mungu hapohapo tuwe vyombo vya kutoa huruma kwa wengine. Kama hatufanyi matendo ya huruma kwa wengine tusitegemee kamwe kupata huruma ya Mungu”.

Ameongeza kuwa huruma ya Mungu ni njia mbili zinazotegemezana na kufanikishana, yaani Mungu anatoa Huruma yake kwa binadamu  ambao nao hawana budi kutoa huruma kwa wanadamu wenzao hasa katika yale maeneo         magumu       na yaliyosahaulika.


 “Nina amini kwamba wakristo wote wa Kahama ambao ni wahitaji wakubwa wa huruma ya Mungu; watakuwa na neema na furaha ya kujitambua na kuzaa matunda mengi na mazuri ya huruma ya Mungu”, amesema.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU