Posts

Showing posts from May, 2019

Papa: Tunafanyia uchunguzi kashfa ndani ya Kanisa

Image
BAba Mtakatifu Francisko katika mahojiano maalum na Kituo cha Televisheni cha Taifa nchini Mexico hivi karibuni pamoja na mambo mengine amezungumzia mauaji ya wanawake ndani ya familia, ukarimu kwa wakimbizi na wahamiaji; uhusiano kati ya siasa na uchumi; madhara ya biashara na matumizi haramu ya dawa za kulevya pamoja na kashfa ya nyanyaso za kijinsia dhidi ya watoto wadogo. Hii ni sehemu ya tafakari ya kina kuhusu hali halisi ya kimataifa sanjari na maisha na utume wa Kanisa kadiri anavyoufahamu Baba Mtakatifu Fransisko. Kuhusu shutuma za kashfa mbali mbali zinazoendelea kujitokeza ndani ya Kanisa, Baba Mtakatifu amesema kuwa, wanazifanyia kazi na kwamba, si kila kitu lazima kitolewe hadharani. Lazima uchunguzi ufanyike na kujiridhisha. Pia Kanisa lina nidhamu ya kuendesha kashfa na kwamba halifanyii kazi story za mitandao na maneno ya kuambiwa. Lazima lifanye uchunguzi wa kina. Jambo la msingi ni watu kuwa na uvumilivu, ili kutoa nafasi kwa viongozi wa Kanisa kufanya uchun

Mkatoliki anayepokea rushwa anaikana imani yake-Ask. Kassala amesema

Image
Na Jimmy mahundi, Mtwara MAkamu wa Rais Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Askofu Flavian Kassala amewataka waamini wa Kanisa Katoliki kuiishi imani yao inayomtaka mkristo kuwajibika kwa uadilifu, kuichukia dhambi yakiwemo masuala ya rushwa. Amesema hayo wakati wa adhimisho la Misa Takatifu ya Jumapili ya 6 ya Pasaka katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Watakatifu wote la Jimbo Katoliki Mtwara Ametaja baadhi ya mambo ambayo yamekuwa kikwazo katika imani   ikiwemo, rushwa, udini,ukabila na umaeneo ambayo vyote hivyo vimekuwa sababu ya mateso kwa wanadamu wengi katika nyakati hizi na matokeo yake ni kushuka kwa imani miongoni mwa waamini. “Haiwezekani jana umepokea rushwa kwa mtu mmoja na leo umekaa karibu naye kanisani halafu wakati wa kutakiana amani mnashikana mikono ya amani!,” amesema Askofu Kassala Kufuatia hali hiyo amewataka waamini kote nchi kuishi kwa kuzingatia imani yao inayokataza rushwa, chuki, ubaguzi wa dini, rangi, kabila, maeneo nk. “Imani yetu inasisi

Ask. Kinyaiya:Acheni kuwatafuta masangoma wakati ninyi ni wakristo

Image
Na Rodrick Minja, Dodoma ASkofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki   Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya, amewaonya baadhi ya waamini wenye tabia ya kwenda kwa waganga wa kienyeji kupeleka matatizo yao. Amewataka   kuachana na imani hiyo mara moja. Ametoa kauli hiyo   kwenye Ibada ya Misa Takatifu alipokuwa anatoa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara   kwa vijana 82 wa Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Wakristo   Kizota Jimboni Dodoma. Askofu Kinyaiya amesema kwa kufanya hivyo muumini anakengeuka na hawezi kuishika imani yake vilivyo kwani atakuwa unatangatanga kiimani. “Tafadhalini sana ndugu zangu tuachane na imani hizo kwa wale wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji, Yesu ndiye kila kitu,”amesema Askofu Mkuu Kinyaiya. Askofu Kinyaiya, amewaasa vijana waliopokea sakramenti ya kipaimara kuwa askari hodari wa Yesu Kristo kwa kuilinda na kuitetea imani yao. Aidha amewataka vijana hao kuwa waaminifu na wajiandae kupokea masakramenti mengine yaliyobaki ya ndoa na utawa/ Upadri kwa wale