Posts

Showing posts from July, 2018

Naibu Waziri Kwandikwa atoa msaada katika shule ya Jimbo la kahama

Image
Na Patrick Mabula, Kahama. NAIBU waziri wa Ujenzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa na Mbunge wa Jimbo la Ushetu , Wilaya Kahama amelishukuru   Kanisa Katoliki   kwa mchango wake katika kutoa huduma za jamii ikiwemo afya na elimu. Amesema hayo alipotembelea shule hiyo hivi karibuni katika ziara yake mjini Kahama ili kutekeleza ahadi yake aliyoitoa kwa shule hiyo   alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kwanza ya wahitumu wa darasa la saba mwaka 2016. Hivyo ameambatanisha shukrani hizo kwa kutoa msaada wa komputa mbili zenye thamani ya shilingi 2,000,000 katika shule ya msingi ya Mtakatifu Athony wa Padua ya jimbo Katoliki Kahama. “Serikali   inatambua mchango wa Kanisa katika huduma   za jamii. Nami ninawashukuru sana kwa kazi hiyo ya kuunga mkono jitihada   za serikali. Nami ninaunga mkono jitihada zenu kwa kidogo nilichotoa ili kwa pamoja tulijenge taifa letu,” amesema. Kwa upande wao watoto wanaosoma shule ya hiyo ya Mtakatifu Athony wa Padua   wamemshukuru waziri

VAZI RASMI LA JUBILEI MIAKA 150 YA UKRISTO

Image
Kamera yetu imewanasa baadhi ya waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Kanisa Kigurunyembe, Jimbo Katoliki Morogoro wakiwa wamevalia nguo za kitenge ambacho ndilo vazi rasmi katika kuadhimisha Jubilei ya miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara, ambapo kilele chake kitakuwa Novemba 4, 2018 kule Bagamoyo. Hakika mama zetu hawa wamelitendea haki vazi hilo na hasa kwa mitindo mbalimbali waliyoshona kama inavyoonekana pichani. Unasubiri nini kujipatia kitenge hicho kwa ajili ya familia yako? Kinapatikana Kurugenzi ya Mawasiliano Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Kurasini jijini Dar es salaam. Weka oda yako kwa kupiga 0657835343 .

Dkt. Kikwete hatalisahau Kanisa Katoliki-Ridhiwani

Image
Na Pascal Mwanache LIKIELEKEA katika kufanya kilele cha Jubilei ya miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara hapo Novemba 4, 2018, imeelezwa kuwa uwepo wa Kanisa Katoliki nchini na ujio wa wamisionari umekuwa mkombozi wa watanzania hasa katika sekta ya elimu na afya, ambapo familia ya Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete imeweka wazi kuwa haitalisahau Kanisa Katoliki. Hayo yameelezwa na Mbunge wa Chalinze na mtoto wa Dkt. Kikwete, Ridhiwani Kikwete, wakati akiongea na waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Kanisa Kigurunyembe Jimbo Katoliki Morogoro, wakati wa Misa Takatifu ya Kutabaruku Kanisa hilo. “Babu yangu mzee Mrisho Kikwete, ambaye kwa ufundi na utaalamu wake alioupata katika Kanisa Katoliki, hata walipokuja watawala wa kijerumani walimuona anafaa kuwa mmoja wa viongozi. Akachaguliwa kuwa wakili wa wajerumani katika shughuli zao pwani ya Afrika Mashariki, hata baadaye wanawe wakasoma katika mfumo huo huo hata wajukuu