Posts

Showing posts from January, 2019

UJUMBE WA BABA MTAKATIFU KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA WAGONJWA DUNIANI FEBRUARI 11, 2019

Image
“MLIPOKEA BILA MALIPO, TOENI BILA MALIPO” (MT.10:8) Wapendwa Kaka na dada zangu, “Mlipokea bila malipo, toeni bila malipo”(Mt 10:8). Hayo ni maneno yaliyotamkwa na Yesu Kristu alipowatuma mitume wake kwenda kueneza Injili,ili ufalme wake uweze kuenea kupitia matendo ya ukarimu na upendo. Mlipokea bila malipo, toeni bila malipo (Mt 10:8). Katika kuadhimisha Siku ya Wagonjwa Duniani, itakayoadhimishwa rasmi tarehe 11-2-2019 huko Calcutta, India, Kanisa- kama Mama kwa watoto wake wote, na hasa walio wagonjwa, linatukumbusha kuwa ishara ya ukarimu na upendo kama wa yule Msamaria Mwema kama njia thabiti ya Uinjilishaji. Kuwajali na kuwatunza wajonjwa inahitaji utaalamu, upole, unyoofu na unyenyekevu unaotolewa bila kujibakiza, matunzo yanayomfanya yule anaye hudumiwa kuonja kupendwa. Maisha ni zawadi kutoka kwa Mungu.Mt. Paulo anauliza “ Ni kitu gani ulicho nacho ambacho hukupokea? (Kor. 4:7). Ni ukweli na dhahiri kabisa kwa sababu ulicho na ulichonacho ni zawadi, maish

JOB OPPORTUNITY/VACANCY

Image

Moto wateketeza nyumba ya Mapadri Walezi wa Seminari Kuu ya Segerea

Image
Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam M oto     umeteketeza   nyumba ya mapadri majalimu na walezi katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Karoli Lwanga-Segerea iliyoko jijini Dar es Salaam majira ya saa nne na nusu usiku Januari 15 mwaka 2019. Kwa mujibu wa Gombera wa Seminari   hiyo Padri Tobias Ndabhatinya chanzo cha moto ni tatizo la umeme lililosababishwa umeme kurudi kwa nguvu baada ya kukatika. “Ni kawaida yetu kila jumatano jioni tunakutana ili kushirikishana masuala mbalimbali ya maisha yetu pamoja na kazi zetu. Wakati tunaendelea na   hilo ghafla tukasikia harufu ya kitu kinachoungua na baada ya sekunde chache tukasikia mlio kama kitu kilicholipuka. Kumbe ulikuwa ni moto ambao umeshaanza kuwaka kwenye ghorofa ya kwanza, ambapo kuna vyumba vyetu vya kulala. Ndipo tukasaidiana pamoja na wanafunzi kutoka nje na kusaidia wale waliokuwa vyumbani washuke. Kisha tukawasiliana na Jeshi la Zima Moto ambalo lilifanya kazi yake hadi kuzima moto huo,” ameeleza Gombera Tobias. Amesema