Posts

Showing posts from June, 2017

“WAWATA HIMIZENI MIITO”

Image
WITO  umetolewa kwa   wanawake  wakatoliki nchini  kuhimiza miito mitakatifu  kuanzia ngazi za familia, jumuiya ndogo ndogo,vigango, parokia hadi  majimboni ili Kanisa liweze kupata hazina kubwa ya mapadri na masista watakaolitumikia kimwili na kiroho pamoja na  watu wake. Aidha imeelezwa kuwa  mapadri na masista  waliopo umri unazidi kuongezeka na hivyo Kanisa linahitaji vijana wa kike na kiume  watakaoandaliwa  katika malezi na kusomeshwa  katika  Seminari  mbalimbali ili waweze kushika majukumu ya kichungaji na kitume katika Kanisa mahalia. Hayo yamesemwa na Katibu  wa Wanawake Wakatoliki Taifa(WAWATA) ambaye pia ni  Mwenyekiti wa WAWATA Jimbo Kuu Dar es Salaam, Bi.Desderia Mahita  wakati  wa hitimisho la Kongamano la siku  tatu la Kanda ya Nyanda za Juu Kusini  lililofanyika jimboni Mbeya na kuwashirikisha  wanawake  wa majimbo 8 ya Jimbo Kuu Katoliki Songea. Majimbo ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini katika Jimbo Kuu Songea  yaliyoshiriki katika  Kongamano hilo  t

TUMUUNGE MKONO RAIS SUALA LA MIMBA SHULENI-ASKOFU KASSALA

Image
Askofu wa Jimbo Katoliki Geita Mhashamu Flavian Kassala amewataka mapadri kutoogopa kusema ukweli ili kuiepusha jamii ya Tanzania kuanguka kimaadili, hasa kwa baadhi ya watu kuilazimisha jamii kufanya mambo haramu kwa kisingizio cha haki za binadamu. Aidha Askofu Kassala ameshangazwa na baadhi ya wazazi wanaopingana na hatua ya Serikali ya kuwanusuru mabinti walio shuleni dhidi ya mimba za shuleni na magonjwa. Askofu Kassala amewaomba wananchi kumuunga mkono na si kumbeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli kwa ujasiri wake kukemea mambo yanayosababisha kumomonyoka kwa maadili nchini. Akizungumza katika Misa Takatifu ya kuadhimisha miaka 25 ya Upadri kwa mapadri wawili wa Jimbo   Geita,  Revocatus Makonge na Deusdedit Kaigoma jumapili iliyopita, Askofu Kassala amemsifu Rais wa Tanzania kwa kusimamia ukweli kuhusu ongezeko la vitendo vya watoto wa shule kubeba mimba na utoaji mimba. "Ni kitendo cha aibu kwa watanzania, wazazi na baadh

“MAKATEKISTA WATHAMINIWE” ASKOFU KYARUZI

Image
Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga Mhashamu Damian Kyaruzi amewataka wakristo nchini kujali na kuthamini utume unaofanywa na makatekista nchini kwani una mchango mkubwa katika kukuza na kutetea imani ndani ya Kanisa. Ameyasema hayo juma hili wakati wa maadhimisho ya misa ya kuwatuma makatekista watatu waliohitimu masomo yao kutoka katika majimbo ya Mpanda na Sumbawanga katika kituo cha malezi cha Mt. Augustino kilichopo Matai jimboni Sumbawanga. “Makatekista ni muhimu na wanahitajika katika Kanisa ukilinganisha na uhaba wa mapadri tulionao, na ukatekista ni wito na wito lazima upaliliwe, mapadri na walei tuwathamini hawa watu ili waweze kututumikia katika mahitaji yetu ya kiroho”. Amesema Askofu Kyaruzi. Askofu Kyaruzi amewataka makatekista kutumika kikamilifu kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake kwa kuimarisha imani za wakristo kwa kukumbuka viapo na kutenda kazi ya bwana wakisaidiana, kutiana nguvu na wenza wao ili kutekeleza wajibu huo kwa kutambua ku

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ALIPONGEZA KANISA KATOLIKI

Image
Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2017 Bw. Amour Ahmad Amour amelipongeza Jimbo Katoliki Ifakara kwa kuendeleza mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Good Samaritan kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wa Kansa iliyopo katika Halmashauri ya mji wa Ifakara. Bw. Amour amesema hayo hivi karibuni kwenye Msafara wa Mwenge wa Uhuru ulipofika katika eneo la ujenzi wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi ambapo ujenzi huo unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Desemba mwaka huu. Aidha Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge Kitaifa kwa mwaka huu amesema kuwa kukamilika kwa Hospitali hiyo kutasaidia watu wengi kupata huduma kwa urahisi kwani huduma zitakuwa zikitolewa bila malipo   ambapo wananchi wengi wenye matatizo ya Kansa kutoka maeneo yote nchini watahudumiwa bure wakiwa hospitalini hapo. “Nawapongeza sana na nawaomba msichoke kufanya vitu vizuri kama hivi, kwani kukamilika hapa kutasaidia wananchi wa Ifakara, Kilombero, Morogoro na Tanzania nzima tena kuna watu wengine watatoka k