Makinikia: Askofu Msonganzila ampongeza Rais Magufuli



Askofu wa Jimbo Katoliki Musoma Mhashamu Michael Msonganzila amesema kuwa kilichojitokeza kwenye ripoti ya pili ya mchanga wa dhahabu ni kwa sababu wahusika wa pande zote mbili hawakuwa makini katika kuona umuhimu wa kumwendeleza mwanadamu kutoka pale alipo.

Askofu Msonganzila ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akitoa maoni yake juu ya ripoti ya pili ya mchanga wa dhahabu iliyowasilishwa hivi karibuni na kamati iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kuwasilishwa Juni 12 mwaka huu.

Amesema wahusika hao wangemakinika katika kuangalia namna ya kumsaidia mwanadamu kiuchumi badala ya kipaumbele chao kikubwa kuwa ni kuchuma pesa bila kumwangalia mwanadamu atanufaikaje na uwepo wa rasilimali hiyo tuliyopewa zawadi na Mwenyezi Mungu katika nchi yetu.

“Binafsi nampongeza Rais Magufuli na ninamuunga mkono kwa hili alilolifanya, amekuwa makini katika kuibua sakata la makanikia, mzalendo wa nchi yake na mtetezi wa wanyonge na nawaomba watanzania tuungane kwa pamoja katika kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wetu,” amesema Askofu Msonganzila.

Askofu amesema kuwa  kinachowaangusha wananchi ni kukosa uzalendo kwa nchi yao na ubinafsi umekuwa mkubwa, na mbaya zaidi  asilimia 10 tu ndiyo ambayo imekuwa ikiliangamiza Taifa, kutokana na kusaini mikataba bila kuisoma, na kwamba sakata hili litumike kumfundisha kila mwananchi kuwa makini wanapotaka kufanya jambo lolote hasa lenye maslahi kwa Taifa.



Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU