Posts

Showing posts from July, 2016

TAMASHA LA MIAKA 20 YA REDIO MARIA,WE AAACHAAAA TU

Image
Kesho(tarehe 30 Julai) ni kesho pale viwanja vya Msimbazi jijini Dsm ambapo Redio Maria itakuwa ikiadhimisha miaka 20 tangu ilipoanizshwa...milima na mabonde ikiinjilisha kwa ubora tena kisasa zaidi....wote mnakaribishwa kushuhudia tukio hili la kihistoria....VIVA REDIO MARIA

VIJANA WANA NAFASI KUBWA KATIKA MABADILIKO

Image
Siku ya Vijana Duniani ni maadhimisho ya imani, matumaini na mapendo kumzunguka Yesu Kristo Mfufuka ambaye yuko kati ya watu wake. Vijana wanahamasishwa kuwa na ari na mwamko mpya wa kutaka kumfuasa, kuishi pamoja na kupyaisha urafiki wao na Kristo Yesu kwa njia ya kuimarisha mahusiano mema kati ya vijana pamoja na huduma makini kwa jirani, ili kuonja na kuonjeshana Injili ya furaha hata katika hali tete za maisha! Ni Kristo Yesu anayewaalika vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia ili kuungana pamoja kuadhimisha Siku ya XXXI ya Vijana Duniani inayoongozwa na kauli mbiu “Heri wenye rehema maana hao watapata rehema”. Heri wenye kusamehe, wenye moyo wa huruma na wanaoweza kujitoa bila ya kujibakiza kwa ajili ya jirani zao. Maadhimisho haya nchini Poland, mahali alipozaliwa Mtakatifu Yohane Paulo II anayeendelea kuwaangalia vijana kutoka mbinguni ili kuonesha ile sura ya huruma ya ujana wa Poland. Maadhimisho haya ni kilele cha Jubilei ya huruma ya Mungu kwa vijana

PAPA ALIPOZURU KAMBI YA MATESO NA MAUAJI

Image
Mama Noemi di Segni, Rais wa Jumuiya za Wayahudi nchini Italia amemwandikia barua Baba Mtakatifu Francisko akimtakia safari njema huko Poland anakokwenda kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2016. Poland ni nchi ambayo imebarikiwa  kwa mambo mengi, lakini pia palikuwa ni mahali ambapo Wayahudi wengi kutoka Italia walikumbana na mateso na hatimaye kuuwawa kikatili kwenye kambi za Auschwitz- Birkenau. Nia ya Baba Mtakatifu Francisko kutembelea katika kambi hizi za mateso katika hali ya ukimya, ili aweze kupata nafasi ya kulia peke yake dhidi ya ukatili wa utu na heshima ya binadamu ni tukio ambalo linasubiriwa na watu wengi duniani. Huu ni ukurasa mchungu wa historia na donda ambalo liko wazi katika historia ya Bara la Ulaya. Ni tukio ambalo linaendelea kusuta dhamiri za watu wengi duniani kuhusu umuhimu wa kusimama kidete kulinda na kudumisha misingi ya haki, amani, uhuru na demokrasia ya kweli. Mama Noemi di Segni anapenda kumpongeza B

Dumisheni utamaduni wa ukarimu na huduma kwa wagonjwa!

Image
Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa, tarehe 29 Julai 2016 akiwa nchini Poland kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya XXXI ya Vijana Duniani ametembelea na kuwasalimia watoto waliolazwa kwenye Hospitali ya Watoto ya Prokocim, Jimbo kuu la Cracovia, kama kielelezo cha uwepo wake wa karibu kwa watoto wagonjwa sehemu mbali mbali za dunia. Akiungana na wote waliofuatana naye, anapenda kuwasikiliza watoto katika shida na mahangaiko yao katika hali ya ukimya, hata kama hana majibu ya mkato! Jambo la msingi ni kusali pamoja nao! Maandiko Matakatifu yanaonesha kwamba, Yesu katika maisha na utume wake alikutana, aliwapokea na kuwakaribisha wagonjwa na wakati mwingine aliwafuata huko walikokuwa ili kukutana nao, kuwaonesha na hatimaye, kuwaonjesha huruma na upendo wake kama mama mzazi afanyavyo kwa mtoto wake. Baba Mtakatifu anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi mema kuonesha ukaribu, huruma na upendo kwa wagonjwa; kwa njia ya ukimya na sala ili kujenga na kudumisha

PAPA ATOA UJUMBE MZITO

Image
Bwana uwahurumie watu wako! Bwana wasamehe kutokana na ukatili huu! Ni maneno ambayo yameandikwa na Baba Mtakatifu Francisko, Ijuamaa, tarehe 29 Julai 2016 kwenye Kitabu cha wageni mashuhuri kwenye Kambi ya mateso na mauaji ya Auschwitz. Katika hali ya ukimya, Baba Mtakatifu ametembelea Ukuta wa kifo, mahali pa mateso na mauaji ya kinazi. Baba Mtakatifu pia ametembelea chumba cha njaa na mahali alipofungwa na hatimaye kuuwawa kikatili Mtakatifu Marximilliano Maria Kolbe, takribani miaka 75 iliyopita. Baba Mtakatifu ametembelea pia kambi ya Birkenau, umbali wa kilometa tatu kutoka kambi ya Auschwitz. Ni mahali ambapo maiti ya waliouwawa kikatili ilikuwa ikichomwa moto. Hapa wafungwa walihukumia kifo cha taratibu. Mwishoni Baba Mtakatifu katika hali ya ukimya na majonzi makuu alitembelea mnara wa kumbu kumbu ya kimataifa uliojengwa kunako mwaka 1967, mahali ambapo kunaonesha kilio cha watu waliokata tamaa, mahali ambapo zaidi ya watu millioni 1. 5 waliuwawa kikatili

MAGAZETINI LEO JUMAMOSI JULAI 30

Image

PAPA AWAAMBIA VIJANA"HURUMA INA SURA YA UJANA"

Image
Pope Francis reached out to over a million young people gathered at Krakow's Blonia Park on Thursday urging them to share God's merciful love. He was speaking during a welcome ceremony for young people attending the 31st World Youth Day in a giant park near Krakow.

PAPA AADHIMISHA IBADA MIAKA 1050 UKRISTO POLAND.

Image
Baba Mtakatifu Francisko Alhamisi, tarehe 28 Julai 2016 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Madhabahu ya Jasna Gòra kama sehemu ya kilele cha Jubilei ya miaka 1050 ya Ukristo nchini Poland, ibada ambayo imehudhuriwa na umati mkubw wa familia ya Mungu kutoka ndani na nje ya Poland wakati huu wa maadhimisho ya Siku ya XXXI ya Vijana Duniani. Akiwa njiani kuelekea kwenye maadhimisho haya, Baba Mtakatifu alipata nafasi ya kuwasalimia Watawa wa Shirika la kutolewa Bikira Maria Jimbo kuu la Cracovia. Baba Mtakatifu katika mahubiri yake kwenye Ibada hii ya Misa Takatifu ametafakari kuhusu Fumbo la Umwilisho, Neno wa Mungu alipofanyika mwili, akaja kukaa kati ya watu wake, lakini kwa bahati mbaya watu wake hawakumpokea. Lakini Mwenyezi Mungu ni mwingi wa huruma na mapendo, wakati ulipotimia, akaujaza ulimwengu kwa wena na huruma yake na hapo akazaliwa Mwana wa Mungu katika hali ya umaskini na unyenyekevu mkuu. Yesu aliwafunulia watu huruma ya Mungu kwa kutenda miuj

WHEN POPE ARRIVED IN POLAND...

Image
Vatican Radio) Pope Francis has arrived in Poland at the start of a five-day apostolic journey. It’s his 15th pastoral visit abroad and features many highlights including participation in the 31st World Youth Day taking place in Krakow, where he will lead a ‘Via Crucis’,celebrate the closing Mass and meet with some of the tens of thousands of young people from across the globe in various occasions. During his visit the Pope will also visit the former Nazi concentration camp of Auschwitz-Birkenau, he will celebrate Holy Mass at the nation's holiest shrine at Jasna Gora and he will pray at the Shrine of Divine Mercy. After landing in Krakow this afternoon Pope Francis addressed the country’s political leaders and urged them to welcome migrants fleeing from wars and hunger. Vatican Radio’s Lydia O’Kane is in Poland reporting on the Pope’s visit. She speaks about his first steps on Polish soil and about the reception he is receiving…

Pope Francis pays tribute to WYD volunteer

Image
(Vatican Radio)  During his stay in Krakow the Holy Father will be residing at the Archbishop’s residence in the heart of the city.  This was the home of the Cardinal Archbishop of Krakow, Karol Wojtyla before his elevation to the See of Peter.  It was from the window of this residence that Pope John Paul II greeted his fellow countrymen on his many papal visits over the course of his pontificate and on Wednesday evening Pope Francis continued that tradition speaking to crowds of young people below. He told them he could see that they were here with great joy in their hearts. Then he said to them that he had some bad news to tell them. Let us be silent, the Pope said, as he spoke to them about a 22 year old WYD volunteer who died on the 2nd of July of cancer having been diagnosed in November of last year. This boy, the Holy Father said had worked very hard for this World Youth Day and had even booked to travel with him on a tram ride during this festival. The

PAPA ASEMA DUNIA IPO VITANI,VITA YA MADARAKA

Image
(Vatican Radio)  Referring to recent acts of violence including the killing of a priest in France, Pope Francis said on Wednesday that the world is at war but stressed “it is not a war of religions but for power. "There is one word I wish to say to clarify." "When I speak about "war" I'm speaking about a war for real, not a "war of religions." It is," he continued, “a war about (economic) interests, money, natural resources and the domination of peoples." All religions, he said, "desire peace. Other people want war." Right!" The Pope was speaking to journalists accompanying him on the plane from Rome to Krakow in Poland.   Pope Francis began his remarks by noting that the word which is being repeated very often now is “insecurity” but, he said, the real word is “war.”  The world is at war, a piecemeal war. There was the 1914 war with its methods, then the 1939-45 one and now t

UFUNGUZI SIKU YA 31 YA VIJANA DUNIANI

Image
Baada ya maandalizi ya kiroho kwa muda wa miaka mitatu, hatimaye, maadhimisho ya Siku ya XXXI ya Vijana Duniani kwa mwaka 2016, huko Cracovia, Poland yanayoongozwa na kauli mbiu “Heri wenye rehema maana hao watapata rehema” yamezinduliwa rasmi na Kardinali Stanislaw Dziwisz, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Cracovia nchini Poland kwa Ibada ya Misa Takatìfu. Vijana kutoka sehemu mbali mbali za dunia wako Poland kuzungumza lugha ya Injili, inayofumbatwa katika upendo, udugu, mshikamano na amani. Wako Jimbo kuu la Cracovia mahali alipozaliwa Mtakatifu Yohane Paulo II, Muasisi wa Siku ya Vijana Duniani, ili kufuata nyayo zake katika kutangaza na kushuhudia Injili na zawadi ya huruma ya Mungu. Hiki ni kipindi cha Sala, Tafakari ya Neno la Mungu na Sakramenti za Kanisa. Katika mahubiri yake, Kardinali Stanislaw Dziwisz amekazia kwa namna ya pekee: majadiliano na Kristo Yesu; Mahali wanapotoka; mahali walipo kwa sasa na kwamba, ni mambo yepi wanayotarajia baada ya maadhimisho

MAGAZETINI LEO ALHAMISI JULAI 28

Image