Posts

Showing posts from April, 2017

Upotoshaji wa Padri kuoa watolewa ufafanuzi

Image
BAADA ya mitandao ya kijamii pamoja na baadhi ya vyombo mbalimbali vya habari kupotosha kuwa Kanisa Katoliki limemfungisha ndoa padri wake, imefafanuliwa kuwa, Padri akiomba kuondolewa upadri wake anaruhusiwa kuoa. Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki Bukoba Mhashamu Methodius Kilaini ameeleza kuwa,katika wito wa Upadri katika Kanisa Katoliki , mapadri hawaoi na hiyo ni sheria ama nidhamu ya Kanisa siyo ya Mungu hivyo Papa ana uwezo wa kuitengua. “Katika Kanisa Katoliki Padri ni kasisi, ni kuhani anayetolea sadaka altareni. Kutokana na nidhamu ya Kanisa Padri haruhusiwi kuoa lakini pale anaposhindwa kuendelea na wito wake ama anapoonekana kwamba anashindwa kuuishi upadri wake anaruhusiwa kuomba kuacha na anaruhusiwa kulingana na taratibu za Kanisa. Mapadri ambao mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vya habari vinazungumzia siyo mapadri walishafuata taratibu zote na kupata kibali kutoka kwa Baba Mtakatifu kuwa wamefunguliwa na upadri wao umeondolewa hivyo wana uhuru wa kuoa kwani

Askofu Mkude aiasa jamii kujitegemea

Image
MOROGORO, Jamii imetakiwa kuwa na moyo wa kujitoa kwa hiyari ili kuchangia huduma mbalimbali na kuonyesha nia yakutatua tatizo badala ya kusubiri kushurutishwa au lifanywe na serikali wakati jamii husika ina uwezo wa kulitatua ikiwa na dhamira. Hayo ameyasema Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro Mhashamu Telesphor  Mkude alipokuwa akihubiri katika parokia teule ya Mtakatifu Josephine Bakita wa Shirika la Stigimatine iliyo Nanenane, ibada iliyoambatana na harambee ya kuchangia ujenzi wa nyumba ya Padri. Askofu Mkude amesema jamii inapaswa kujitoa na siyo kusubiri ifanyiwe kila kitu ikiwa watu kwa utashi waliopewa na Mungu wana uwezo wa kusimama na kufanya pasipo kutegemea nguvu ya mtu mwingine iwainue. “Jamii inapaswa kujitoa na siyo kusubiria kufanyiwa kila kitu, ikiwa sisi wenyewe tuna uwezo wa kusimama na kufanya pasipo kutegemea nguvu ya mtu mwingine aje atuinue, kwa kufanya hivyo ni kushusha ule utashi ambao Mungu ametupatia na kujiona wanyonge tusioweza kufanya chochote,” am

Geita waandaa Hija ya Miaka 100 ya Upadri

Jimbo Katoliki Geita linatarajia kuhitimisha Jubilei ya miaka 100 ya Upadri Kijimbo kwa Hija ya aina yake itakayoambatana na Misa Takatifu itakayoongozwa na Askofu wa Jimbo hilo Mhashamu Flavian Kassala katika Parokia ya Nyantakubwa kwenye eneo lenye masalia ya Mmisionari wa kwanza. Akitangaza tukio hilo hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kamati ya Hija, Padri George Nkombolwa amesema pamoja na kwamba maadhimisho ya kuenzi miaka 100 ya upadri Tanzania Bara kijimbo yamepewa uzito mkubwa kwa sababu mmoja wa mapadri wanne wa kwanza wazalendo, (Pd. Angelo Mwilabure) alitokea Jimboni Geita katika Parokia ya Kome-Nyakasasa, Jimbo pia lina Misioni Kongwe iliyoanzishwa miaka ya 1880 na mapadri wa Shirika la White Fathers, ambapo mmoja wao, Padri Mfaransa "Combarieu"alizikwa na masalia yake yanasadikika kuwepo maeneo hayo. Padri Nkombolwa ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Nyantakubwa amesema uwepo wa Misioni Kongwe kupita zote kwa upande wa Kusini mwa ziwa Victoria, iliyojulikana 

Kongamano la Utoto Mtakatifu (Haki na Amani) kufanyika Juni Zanzibar

Image
Kongamano la utoto Mtakatifu-Watoto wa Haki na Amani linatarajiwa kufanyika Jimboni Zanzibar kuanzia tarehe 8-11 Juni mwaka huu. Hayo yamesemwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Zanzibar Mhashamu Augustine N.Shao C.S.Sp hivi karibuni ambapo amewaalika waaamini kuwaandaa watoto kwa ajili ya Kongamano hilo. Askofu Shao amesema Kongamano hili ni sehemu ya Umisionari wa Watoto kwa watoto wenzao   wa Zanzibar na wakristo kwa ujumla. Katika Kongamano hilo watoto wataonesha vipawa vyao katika kumsifu Mungu, kushirikishana zawadi walizojaliwa na Mwenyezi Mungu katika michezo, sala na kufurahia kwa pamoja kama familia. Askofu Shao ameomba waamini waungane na watoto hao katika kusali na kuiombea Dunia amani ambayo ni lazima ianzie kwenye familia na kuwa na umoja. Kauli mbiu ya kongamano hilo ni “UPENDO NA MSAMAHA UHAI WA FAMILIA” ambayo imejikita katika kutafakari nguvu ya msalaba na Neno la Mungu. “Kristo amekuja ili tuwe na uhai tena tuwe nao kamili” (Jn.10:10) Wakati huohuo, Paro

Jamii Manyoni yaaswa kuwathamini watoto yatima

MRATIBU wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Manyoni Orphans Sponsorship Association (MOSA) kilichopo wilayani Manyoni mkoani Singida Bi.Mahewa Mowo ametoa wito kwa jamii kuwajali na kujitolea kuwapenda watoto yatima. Mratibu huyo ametoa kauli hiyo hivi karibuni kituoni hapo alipotembelewa na gazeti hili na kufanya mahojiano maalumu yenye lengo la kuikumbusha jamii juu ya watoto yatima. Hata hivyo mratibu huyo amesema kuwa jamii inajisahau na kuutupa utu wa mtoto yatima huku baadhi yao wakitendewa vitendo viovu na walezi wao ikiwa ni pamoja na kuwanyima haki ya kupata elimu. "Jamii imejisahau sana na kuutupa utu wa mtoto yatima ,tafadhali tusiwatenge ili wasijione wapweke, tupo kwa ajili yao," amesema. Pamoja na hayo Bi.Mowo amesema mtoto yatima ni mtoto wa jamii na hivyo jamii inapaswa kumwangalia kwa ukaribu ili kutimiza mapenzi ya Mwenyezi Mungu ya kumpenda jirani yako kama nafsi yako. “Watoto yatima ni wa jamii nzima, hatupaswi kuwabagua wala kuwany