Askofu Mkuu Marek ateuliwa Balozi wa Vatikani nchini Tanzania

BABA Mtakatifu Fransisko amemteua Askofu Mkuu Marek Solczyński kuwa Balozi mpya wa Vatikani nchini Tanzania. Kabla ya uteuzi huu, Askofu Mkuu Solczyński alikuwa Balozi wa Vatikani nchini Georgia, Armenia na Azerbaijan.

Itakumbukwa kwamba, Askofu Mkuu Solczyński alizaliwa Aprili 7, 1961 huko Stawiszyn, nchini Poland. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, mnamo Mei 28, 1987 akapewa Daraja Takatifu ya Upadri.


Baada ya kufanya utume wake katika masuala ya diplomasia sehemu mbali mbali, tarehe 26 Novemba 2011, Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI akamteuwa kuwa Askofu Mkuu na kumwekwa wakfu tarehe 6 Januari 2012. Askofu mkuu Marek Solczyński ameshiriki kikamilifu katika maandalizi ya hija ya kitume ya Baba Mtakatifu Fransisko nchini Georgia, Armenia na Azerbaijan aliyoitekeleza mwaka 2016.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU