UZINDUZI WA KONGAMANO LA VIJANA KITAIFA JIMBO KATOLIKI MOSHI

 Kongamano la Vijana kitaifa limezinduliwa katika Jimbo Katoliki Moshi katika shule ya Sekondari Marangu. Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba Mhashamu Desderius Rwoma amewataka vijana kuwa kioo cha jamii kwa kutenda mema ili kulisaidia taifa katika nyanja mbalimbali. Amewakumbusha kuyajali mazingira, kuwa watiifu, kuzingatia mafunzo ya Kanisa na pia kuiishi miito. Semina mbalimbali zitaendeshwa kwa vijana katika Kongamano hilo hadi kilele chake tarehe 17 Aprili. 

Comments

  1. Nimefurahi kuingia katika tovuti hii leo kwa mara ya kwanza. Ingependeza Zaidi iwapo hizo picha hapo juu zingekuwa na maelezo. Yaanimfano. Hili ni kanisa la kwanza ambalo ni mama wa makanisa yote limejengwa (1843)Bagamoyo. picha inayofuata labda ni Kanisa kuu la Mt Petro Vatican n.k

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU