KUELEKEA KILELE CHA JUBILEI KUU – ARI YA KICHUNGAJI MUHIMU
K atika kuadhimisha Jubilei ya miaka mia moja na hamsini ya Uinjilishaji, Kanisa Katoliki Tanzania linamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuwatuma Wamisionari kuja kutangaza Injili Tanzania. Kwa kuzingatia jinsi Wamisionari walivyojitoa katika kutangaza Injili, na kupambana na changamoto mbalimbali, Kanisa la Tanzania linapaswa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa Uinjilishaji wa miaka hiyo mia na hamsini. Awamu za Uinjilishaji Wataalamu wa historia hutueleza kwamba katika Afrika ya Mashariki, Uinjilishaji wa kwanza ulifanywa na Wamisionari wa shirika la Mtakatifu Agustino mnamo mwishoni mwa karne ya kumi na tano. Wamisionari hao walifuatana na mvumbuzi mashuhuri aitwaye Vasco da Gama, na walifika Zanzibari 1499 na lengo lake lilikuwa kutafuta njia ya kwenda India na mashariki ya mbali. Katika kuinjilisha, wamisionari hao walipata upinzani mkubwa kutoka kwa Waarabu. Walijitahidi kuendelea lakini mnamo mwaka 1698 Uinjilishaji huo ni kama ulififia. Sababu kubwa ya...