Posts

Showing posts from April, 2018

‘Bila ushirikiano wa Serikali na Kanisa hakuna maendeleo’

Image
Na Izack Mwacha Singida ASKOFU wa Jimbo Katoliki Singida Mhashamu Edward Mapunda, ameipongeza serikali ya Mkoa wa Singida, kwa kutoa ushirikiano na Kanisa katoliki katika shughuli za maendeleo. Askofu Mapunda ameyasema hivi karibuni katika uzinduzi wa miaka 22 ya Radio Maria Tanzania iliyofanyika Parokia ya moyo Mtakatifu wa Yesu Jimbo Katoliki   Singida. Katika homilia yake Askofu Mapunda amesema kuwa ushirikiano ukidumishwa Kati ya serikali na Kanisa ni lazima maendeleo yawepo,kwani miongoni mwa mambo ambayo yanaleta chachu ya Nguvu, umoja na mshikamano ni ushirikiano ambao kwa kiasi kikubwa unaleta hali ya kujaliana, hivyo anategemea maendeleo makubwa zaidi katika Jimbo la singida Askofu mapunda amesisitiza kuwa, ili imani ya Kanisa Katoliki iendelee kudumu zaidi ni lazima kwa kila mkristo mkatoliki mmbatizwa afahamu umuhimu wake wa kuchangia vyombo vinavyoweza kuisambaza injili hiyo kwa kasi zaidi ulimwenguni kote ikiwemo Radio Maria, kwani hiyo ni njia pekee ambayo

Vyombo vya habari vya Katoliki vyaaswa kufahamisha umma juu ya miaka 150 ya uinjilishaji

Image
Na Julieth Muunga Dadi, Dar es Salaam W anamawasiliano wa Vyombo vya Habari vya Kanisa Katoliki wametakiwa kuweka mikakati madhubuti kupitia njia za mawasiliano ikiwemo Televisheni, Radio na Magazeti ili kurahisisha na kuendeleza utume wa Kanisa. Aidha Vyombo hivyo vya habari viweke mikakati madhubuti ili kuelimisha na kufahamisha uma kuhusu Jubilei ya   Miaka 150 ya Ukristo Tanzania. Wito huo umetolewa hivi karibuni na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Raymond Saba wakati akifungua Mkutano   Mkuu wa   Mwaka wa Wakurugenzi wa Mawasiliano Majimboni na wa Vyombo vya Habari vya Kanisa uliofanyika hivi karibuni Kurasini, Jijini Dar es salaam. Padri Saba amesema kuwa,   kama wanamawasiliano hawana budi kuweka mikakati ya kuhamasisha waamini juu ya matukio mbalimbali katika Kanisa ikiwemo Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara. “Ni wajibu wa Vyombo vyetu vya Habari vya Kanisa Katoliki kuhakikisha waaamini wanajua, wana

Dodoma yapewa hadhi ya kuwa jiji

Image
Na Dotto Kwilasa,Dodoma. K ATIKA maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, iliyokuwa halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imepandishwa hadhi na kuwa jiji. Akihutubia wananchi katika sherehe hizo za muungano katika uwanja wa Jamhuri Dodoma hivi karibuni,Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amesema kutokana na mamlaka aliyo nayo anatangaza rasmi kuupa hadhi ya jiji mji wa Dodoma. Pamoja na hayo amesema, kutokana na kuupadisha   mji wa Dodoma kuwa na hadhi ya jiji , hivyo aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ataitwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma hatua   ambayo imeungwa mkono na wananchi waliokuwa uwanjani kusherehekea muungano . Sambamba na hayo amesema dhamira ya serikali kuhamishia makao yake makuu bado ipo pale pale na kwamba zaidi ya watumishi wa serikali 3800 tayari wamehamia Jijini Dodoma. Wakizungumzia hatua hiyo, baadhi ya wananchi mkoani humo wamesema   kutokana na Dodoma kutangazwa kuwa jiji mzunguko wa kibias