Uchaguzi Mkuu kuangukia Jumatano imejibu maombi ya Wakristo – TEC


KATIBU Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padri Charles Kitima, ameielezea hatua ya Serikali kuitangaza Oktoba 28 kuwa tarehe ya kuppiga kura katika Uchaguzi Mkuu nchini,  kwamba imietimiza ombi la muda mrefu la waamini Wakkristo kufuatai tarehe hiyo kuangukia Jumatano ambayo siyo siku ya Kiibada kwao.

Alitoa kauli hiyo  wakati akizungumza na vyombo vya habari, katika mahojiano yaliyofanyika ofisini kwake Kurasini jijini Dar es Salaam, ambapo alisema tofauti na chaguzi zilizopita ambazo zimekuwa zikifanyika siku ya Jumapili, uchaguzi wa mwaka huu umetekeleza kwa vitendo haki ya kila Mtazania kuwa na Uhuru wa kuabudu na uhuru wa kupiga kura.

“Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 5 inaweka wazi haki ya kila Mtazania mwenye sifa zinazotakiwa kushiriki kikamilifu uchaguzi iwe ni kwa kupiga kura au kuchaguliwa huku Ibara ya nane pamoja na mambo mengine, inatoa uhuru wa kujitawala…hivyo uchaguzi wa namna hii kufanyika Jumapili ulikuwa unagonganisha haki msingi za kuabudu na kupiga kura,”


Hata hivyo alipendekeza uamuzi huu huwe endeleavu yaani kwa tarehe ya uchaguzi kuangukia siku ambazo si za Ibada kwa dini na madhehebu yote nchini.

“Leo tusifurahie Wakristo alafu uchaguzi mwingine ukaangukia kwenye siku ambayo wenzetu Waislamu ama Wasababto wanaitumia kuabudu, badala yake tunaomba liwe zoezi endelevu ya kuheshimu siku hizo za kuabudu kwa imani zote,” amesisitiza.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeitangaza Oktoba 28 mwaka huu kuwa siku ya kupiga kura kuwachagua rais, wabunge na madiwani, ikiwa ni Uchaguzi Mkuu wa sita tangu Tanzania iingie kwenye Mfumo wa vyama vingi nchini.

Hata hivyo hii itakuwa ni sehemu ya historia kwani katika chaguzi kadhaa zilizopita, uchaguzi wa mna hiii umekuwa ukifanyika siku ya Jumapili ambayo ni siku ya Kiibada kwa waamini wa Dini ya Kikristo husuani wale ambao wapo chini ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) huku madhebu ya Kisabato yakisali siku ya Jumamosi na upande wa Waislamu wao siku ya ya Ibada ni Ijumaa.

Miongoni mwa chaguzi hizo zilizofanyika Jumapili kwa miaka ya hivi karibuni ni Uchaguzi Mkuu wa 2005 uliofanyika Desemba 4 mwaka huo ambao hata hivyo ulikuwa ufanyike Jumapilipi ya Oktoba 3 mwaka huo lakini ukahairishwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Alli Juma. Mwingine ule wa mwaka 2015 uliofanyikaa Jumapili ya Oktoba 25 mwaka huo.


Comments

  1. Tumsifu Yesu kristu .ninaujumbe wapendwa Mimi nimkatoliki waamini wetu hawajui kusoma biblia wamepumbazwa na shajara .chonde maaskofu .futenikabisa mashajara tuzoeee kushika bibilia.shajarani wakala wampumbaza Kristu.Roho mt.awaongozee 2026 kusiwe na mashajara tena tushike biblia nazaburi zake zitukae.tutaimarika.Asanteni niwazo langu tuuu wapedwaMbarikiwe.

    ReplyDelete
  2. Ukiwa umefanya kazi maisha yako yote kujenga familia na urithi, huwezi kuruhusu kivuli cha mtu wa tatu kiiharibu katika miezi michache tu. Niligundua kuwa mabadiliko ya ghafla ya tabia ya mume wangu yalikuwa kuingiliwa kiroho, si tu mgogoro wa katikati ya maisha.

    Niliwasiliana na Mystic Kakaa kwa ajili ya uingiliaji kati wa kibinafsi. Kazi yake ilikuwa ya upasuaji. Alitambua kivuli na kukiondoa kabisa bila drama yoyote ya umma. Ndani ya siku 5, umakini wa mume wangu ulirudi nyumbani kwetu na katika mustakabali wetu. Ikiwa unalinda maisha yenye thamani kubwa na unahitaji bwana anayeelewa busara, wasiliana naye kwa: dawnacuna314@gmail.com

    WhatsApp: +2349046229159

    Yeye ndiye kiwango cha dhahabu.
    Kwa uchawi wa upatanisho wa uhusiano/ndoa.

    Uchawi wa kumfanya mpenzi wako wa zamani/mwenzi wako aombe msamaha.

    Uchawi wa kumrudisha mpenzi wako/kumvutia mpenzi mpya.

    Uchawi wa kurejesha mali/pesa zilizoibiwa.

    Mabadiliko ya umbo/Uchawi wa kutoweka.

    Uchawi wa kushinda bahati nasibu/kesi ya mahakama. Na zaidi

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

MJUE MTAKATIFU MARIA GORETTI