TAHADHARI YATOLEWA KUELEKEA KONGAMANO LA VIJANA KANDA YA ZIWA GEITA





MLEZI wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (Metropolitani) Kanda ya Mwanza Padri Paschalis Buberwa amewatahadharisha vijana watakaohudhuria kongamano la Kanda kuvaa mavazi yenye maadili.

Kongamano hilo linatarajiwa kuwakusanya takribani vijana wakatoliki 2000 kutoka Kanda ya Jimbo Kuu Mwanza yaani mikoa ya Kanda ya Ziwa ambapo watapata mafundisho ya kiimani, semina za kimaisha kwa ujumla na pia ujasiriamali kuwawezesha vijana kuwa na shughuli za vipato vya kujikimu kimaisha.

Akizungumza katika mkutano wa maandalizi ya Kongamano hilo mapema wiki hii jimboni Geita, Padri Buberwa wa Jimbo Katoliki Bukoba amesema kuwa miongoni mwa mavazi anayohofia kuvaliwa na vijana ni pamoja na suruwali mtepesho, sketi fupi, nguo za kubana kwa wavulana  na wasichana.

Amesema mavazi hayo yanapaswa kukemewa kwa vijana wote, siyo kwenye Kongamano tu bali mahali popote kwa vazi la mtepesho tafsiri yake ni kujitangaza ushoga kwa anayevaa. 

Walezi mbalimbali walikutana katika makao makuu ya Jimbo Katoliki Geita kutoka majimbo ya Mwanza, Shinyanga, Musoma, Geita, Bukoba, Bunda, Rulenge Ngara na Kayanga kuandaa Kongamano hilo litakalofanyika tarehe 15-19 Juni jimboni Geita.

Wajumbe mbalimbali wameonesha matumaini makubwa kwa Kongamano hili lijalo huku wakibainisha kuwa ni fursa pekee ya kuwapatia vijana dira ya kimaisha na kiroho na kwamba linawapatia mwamko mpya juu ya Uinjilishaji wa Vijana katika Kanisa la Tanzania.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU