“Fungeni kabla ya kupokea Ekaristi Takatifu”



Paroko wa parokia ya Chuo Kikuu Dsm Mlimani, Padri Deograthias Mbiku amewataka wakristo kuiheshimu Ekaristi Takatifu kwa kuzingatia kanuni wakati wa kuipokea.
Akizungumza na wakristo waliofurika katika Dominika ya Ekaristi Takatifu katika Parokia ya  Bikira Maria Konsolata Kigamboni Dar es salaam, Monsinyori amesema kila mkristo inampasa kufunga saa moja kabla ya kupokea Ekaristi Takatifu, na baada ya kupokea anaweza kuendelea kula kadri atakavyo.
“Waamini wawe katika neema ya utakaso rohoni yaani mpokeaji asiwe na dhambi ( 1 Paulo 11-27-32), wawe na usafi wa mwili, wawe na imani ya kwenda kumpokea Mungu na mtu asile kitu chochote kabla ya kupokea isipokuwa maji pekee.” Amebainisha.
Wakati huohuo Monsinyori ametoa sakramenti ya kipaimara kwa vijana 238 toka Parokia hiyo na kuwaagiza mambo ya kufanya ikiwa ni pamoja kumshuhudia Kristo katika maisha yao, kutangaza habari njema kwa kila kiumbe na kwa kila Taifa, wasome Biblia na kuijua wakiongozwa na Roho Mtakatifu waliyempokea, wasali kwa bidii zote na watumie karama mbalimbali walizopewa na Mungu kwa maana kila mwanadamu Mungu amempa karama zake.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU