Askofu Ruwa’ichi: Msiabudu mali

Na Dominic Haule, Dar es Salaam
waamini nchini wametakiwa kuacha kuabudu mali zao kama vile biashara, mashamba, ofisi,mifugo mazao nk. badala yake  wamwabudu  Mungu pekee mtoaji wa vyote.
Hayo yamesemwa na Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi  wakati  wa homilia yake  hivi karibuni katika Jubilee ya Miaka 50 ya Updri ya Padri Camille Neuray Paroko wa Parokia ya Mt.karoli Lwanga Yombo Dovya.
“Kinacho tutunza sio mali, bali ni Mungu mwenyewe anaye sitawisha  mali na kuzifanya zizae. Hivyo tunapaswa kumwabudu Mungu na sio kitu kingine chochote,” amesema.
  Amesema kuwa adhimisho la jubilee ni jambo linalobeba maana  kadhaa miongoni wa mambo hayo ni fursa  ya kumshukuru Mungu, kujiweka wakfu upya, kujiaminisha kwake tena kujinyenyekesha na kuomba toba  pamoja na neema na baraka.
Hata hivyo Amesema kuwa watumishi wa Mungu wanatakiwa kuwa kama akina Paulo, Adrea , filipo na wengine waliokuwa mitume wa Yesu kama sehemu ya kuiita miito mitakatifu katika jamii wakiwemo vijana na watoto kuingia katika wito wa utawa Kama Padri Camille Naeuray.
Aidha adhimisho hilo ni ungamo lakiimani kana kwamba bila Mungu hatufanikishi kitu hivyo wanapaswa kumuomba Mungu ili awasaidie kufanikisha kazi aliyowaitia katika wito wa kumtumikia Mungu hapa ulimwenguni.
Askofu Ruwa’ichi amempongeza Padri Camille Neuray katika uaminifu wake wa kudumu katika utume na kujitoa sadaka katika kufanya utume bila kujibakiza.
Pamoja na  kumuombea kila la heri ili aweze kufikia Miaka 50 ya Utume.
Padri Camille Neuray wa Shirika la Wakamilian alianza utume wake wa Upadri  katika  Parokia ya Ngerengere Mkoani Morogoro, Kisha Mt Camillian Kiwalani Dar es sala kwa sasa anaendelea na utume huo katika Parokia Mt.Kaloli Lwanga -Yombo Dovya.
Misa hiyo ya jubilei ya miaka 50 ya updri wa padri Camille Neuray kutoka Parolika ya Mt. Karoli Lwanga Yombo Dovya imeongozwa na Askofu Mkuu Mwandamizi Yuda Thadeus Ruwa’ichi akishirikiana na Monsinyori Mbiku na mapadri wa shirika la wakamilian pamoja na mapadri wa mashirika mengine na mapadri wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU