Kahama wafanya harambee kujenga Chuo cha Ukatekista

Na Patrick Mabula , Kahama.
Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde ametoa wito kwa waamini kuziheshimu alama mbalimbali za imani ndani ya  Kanisa.
 Askofu Minde alitoa wito huo katika homilia aliyotoa katika Misa Takatifu iliyoiadhimisha katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Karoli Lwanga, Parokia ya Kahama mjini  ambapo pia kulikuwa na harambee ya kuchangia ujenzi wa Chuo cha Makatekista jimboni hapa.
Akiongea katika misa hiyo aliwataka waamini kuheshimu alama mbalimbali  za imani  ndani ya kanisa katoliki kuanzia na  Msalaba Mtakatifu  ambayo ndiyo ishara kuu ya  Mkirsito Mkatoliki.
Askofu Minde amesema waamini waache kuona aibu kuwa na Msalaba kuweka katika nyumba zao , biashara na Rozali , kusoma   Bibilia , maji ya Baraka katika familia zetu hizo ndiyo baadhi ya alama ya Mkatoliki lazima tuzionee fahari.
Amesema katika maisha ya imani lazima waamini waendelee kumkumbatia Yesu Kristo , kusoma neno la Mungu , kusali katika familia , jumuiya ndogondogo  na kuhudhulia Misa Takatifu.
Askofu Minde amesema anawapongeza Mababa Mapri , Watawa kwa kazi nzuri wanayofanya katika malezi ya kuwalea waumini kiroho  na kutaka kuendelea kumuomba Mungu  aendelee kutujalia imani.
Mmoja  kati ya waliokuwa wageni rasmi katika harambee hiyo,  Frederick John akiongea baada ya misa alisema anampongeza sana, Askofu Minde kwa kuona umuhimu wa kujenga chuo cha Makateksta  ambao ni wa muhimu sana katika mafundisho ya imani ya Kanisa.
John amesema katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia , Makatekista wanapaswa kujengewa uwezo wa kutosha kutakako wasaidia  kuweza kufundisha vizuri katekismu ya kanisa katoliki.
Amesema mafundisho ya makatekista ndiyo chimbuko la imani pamoja na  miito ya kwenye ndoa, upadri na utawa ndani ya kanisa , kwa hiyo kukamilika  kwa chuo hicho  mwishoni mwa mwaka huu kitawasaidia sana kuwajengea uwezo walimu hao wa dini.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU