Ask. Mlola: Huruma ya Mungu ni nguzo kuu ya Kanisa

ASKOFU wa Jimbo Katoliki Kigoma Mhashamu Joseph Mlola, ALCP/OSS amesema kuwa Huruma ya Mungu ni nguzo kuu ya Kanisa, kwa kuwa hiyo ndiyo  njia inayomuunganisha Mungu na mwanadamu.

Ameeleza hayo wakati wa Ibada ya Misa ya kufunga  Mwaka wa Huruma ya Mungu Kijimbo iliyofanyika Parokiani Kasulu, iliyohudhuriwa na wawakilishi kutoka parokia mbalimbali zilizomo Jimboni Kigoma.

Askofu Mlola amesema kuwa huruma inafungua moyo wa mtu katika matumaini kwa kutambua kwamba, daima anapendwa, licha ya mapungufu na udhaifu wake wa Kibinadamu.

“Huruma ya Mungu ni sheria makini inayojikita katika moyo wa mwanadamu na nguzo inayolisimamisha Kanisa. Katika hili Papa Fransisko naye anakazia umuhimu wa nguvu ya Mungu. Anakiri kwamba, huruma ya Mungu ni ya milele na kwamba, mwanadamu daima ataendelea kuwa chini ya jicho la huruma ya Mwenyezi Mungu” ameeleza

Aidha amebainisha kuwa upendo ni kielelezo cha utendaji wa Mungu na unakuwa ni kielelezo cha kuwatambua watoto wake wa kweli. Ameasa kuwa wakristo wote wana changamoto ya kumwilisha huruma, kwani wao wamekuwa ni watu wa kwanza kuonja huruma, kwa kupata msamaha wa dhambi zilizotendwa, kumbe ni jambo la msingi kwa wakristo kutambua fursa hii.


“Mara nyingi watu wanadhani kwamba, si rahisi kuweza kusamehe, lakini ikumbukwe kwamba, msamaha ni chombo ambacho kimewekwa mikononi mwa binadamu wadhaifu, ili kuweza kupata utulivu moyoni, ili hatimaye, kuishi kwa furaha” amesema.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU