Waamini watakiwa kuwa makini na maendeleo ya teknolojia

WAAMINI wametakiwa  kuwa  makini  juu ya  maendeleo ya sayansi na teknolojia yanayoendelea  duniani  kote  yasije yakawaondoa katika misingi  wa imani  waliyonayo ndani ya Kanisa.

Hayo yamezungumzwa na Askofu Ludovick Minde wa Jimbo Katoliki Kahama alipokuwa akifunga mwezi wa Rozali Takatifu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Karoli Lwanga parokia ya Kahama mjini.


“ Wakristo sasa hivi katika maisha yetu tumezingirwa na mambo mengi katika dunia hii ya sayansi na teknolojia mnapaswa kuwa waagalifu na kusimama imara katika  mafundisho na mapokeo ya Kanisa,” Amesema Askofu Minde.

Askofu Minde aliwataka waumini kukufua moyo wa sala kwa Mama Bikra Maria kwa kila muumini , familia , jumuiya na kwa Kanisa lote katika shida mbalimbali wataweza kushuhudia makuu kwenye maisha yetu ya kila siku.

Alisema sala ya Rozali Takatifu ni alama ya kumshukuru Mungu  kwa zawadi ya Mama Bikra Maria anayetujali fadhili nyingi  binafsi katika mioyoni mwetu , amani familia, jumuiya,  taifa  letu na  kwa kanisa kwa ujumla.


Askofu Minde katika kufunga mwezi wa sala ya Rozali Takatifu  aliwaongoza waamini  wa Kanisa Kuu la  parokia ya Mtakatifu Karoli Lwanga Kahama mjini kusali rozali  mafungu yote kwa maandamo na kisha kumaliza kwa ibada huku akiwaalika kuwa watu wa sala kwa Kristo na Mungu wetu katika kupata wokovu.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU