“Ishini Kitakatifu”- Askofu Ruwa’ichi

WAKRISTO wameaswa  kuchangamkia mambo ya kanisa zaidi na siyo ya malimwengu ili waweze kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza Mungu na kuzingatia utakatifu kama wito wa kila mbatizwa.
Wito huo umetolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi Katika homilia yake kwenye adhimisho la ibada ya misa takatifu ya uzinduzi wa parokia ya NUNDU Jimboni humo.
Askofu Rwai’chi katika ibada hiyo Ametoa “OLE” kwa wale wote wanao wakatisha wakristo wengine tamaa wakati wanapojitahidi kufanya mambo matakatifu huku wakijiona wapofu pamoja na kuwafananisha na watawa.
“Usimkatishe tamaa mtu anayejitahidi kuishi maisha ya kimungu, mbona unafanya mambo matakatifu sana kwani wewe ni mtawa?” Amesema Askofu Ruwai’chi.
Pamoja na hayo Askofu Ruwa’ichi amesema wakristo wamekuwa na tabia ya   kusifiana kwenye mambo madogo madogo hususani ya kidunia badala ya kusifiana katika mambo ya kimungu, wakisahau ya kwamba  wote ni wadhambi.
Akizungumzia siku ya WATAKATIFU WOTE ambayo huazimishwa kila mwaka tarehe mosi Novemba amesema kuazimisha siku hiyo ni tukio kubwa la kikanisa ambalo wakristo wote ulimwenguni huwakumbuka waamini wenzao, wafuasi wa Kristo ambao waliishi ukristo na utume wao kwa dhati bila ya kujibakiza na hivyo baada ya ufuasi wao uliotukuka wakatukuzwa pamoja na Kristo.
  “Nyerere atatangazwa lini Mtakatifu?” hili ni swali ambalo Maaskofu wengi wa nchi za Afrika wanapenda kuniuliza pindi ninapokutana nao kwenye mikutano.

Huu ni mfano mzuri kwa nchi ya Tanzania kwani swali kama hilo linaonyesha dhahiri kwamba mchango wake katika jamii ulionekana hivyo ni vema sana kwa wakristo wote kufanya mambo mengi yatakayowafanya watu wawe na sababu za kuwaona watakatifu na endapo watu hawatayaona utakayokuwa ukiyaishi mwishowe utavikwa taji mbinguni”.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU