Askofu Nzigilwa: Watunzeni Watawa

Askofu msaidizi wa jimbo kuu katoliki Dar es salaam Mhashamu Eusebius Nzigilwa ametoa wito kwa walei wote kuwa ni jukumu lao kuwalea na kuwatunza watawa popote walipo.
Akizungumza katika mahubiri ya misa takatifu iliyofanyika katika parokia ya Mtakatifu Annastazia na Frolian iliyopo Kigamboni Kimbiji(Kidagaa) jijini Dar es salaam, Askofu Nzigilwa ametoa wito kwa waamini kwa kushirikiana na majimbo kuwa bega kwa bega na watawa jambo ambalo litasaidia kurahisisha kazi ya kuitangaza injili.
Askofu Nzigilwa ambaye alikuwa mgeni rasmi parokiani hapo katika uzinduzi wa nyumba mpya za watawa (masista) amewataka walei wa Kimbiji (kidagaa) kuwapokea watawa hao na kuwapa ushirikiano wa hali na mali katika kazi mbalimbali za kijamii na kiimani.
Parokia ya Mtakatifu Annastazia na Frolian inaongozwa na Paroko Luchano na msaidizi wake padri Justus Rugaiyukamu ambapo kwa kipindi kirefu wamekuwa peke yao parokiani hapo.
Parokia hiyo inajumuisha vigango vinne ambavyo ni Mbutu, Buyuni, Puna na Ngobanya.

Askofu Eusebius Nzigilwa pia ametoa sakramenti ya kipaimara kwa vijana wanne parokiani hapo.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU