Ask. Minde awataka waamini kijiandaa kumpokea Mtoto Yesu.
ASKOFU Ludovick Minde wa Jimbo la Katoliki
Kahama amewataka waamini kujitakasa na kujiandaa kiroho katika kipindi
hiki cha maajilio ili waweze kumpokea kwa moyo
safi Masiha Yesu Kristo.
Askofu
Minde ametoa wito huo hivi karibuni katika Misa Takatifu alipokuwa
akizinduzia Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu Lulembela
jimboni humo .
Askofu Minde alisema
Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu , Lulembela aliyoizindua ni moja
ya matunda ya Yubilee ya Mwaka wa Huruma ya
Mungu jimboni humo kwa kuwasogezea karibu waamini huduma
ya kiroho na kichungaji .
Ikumbukwe kuwa, hadi
sasa jimbo la Kahama lina jumla ya
parokia 23.
Comments
Post a Comment