"VIROBA MARUFUKU" WAZIRI MKUU




SERIKALI  imeziagiza kampuni zote  zinazozalisha vinywaji vya pombe kali zenye vibali vyote kubadilisha teknolojia ya ufungaji wake na kuweka vinywaji hivyo kwenye chupa kutoka katika vifungashio vidogo(maarufu viroba) .

Agizo hilo limetolewa mjini hapa hivi karibuni na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, wakati akifungua kikao cha baraza la mawaziri ambacho ni cha kwanza kufanyika mkoani Dodoma baada ya serikali kuhamia Dodoma.

Hata hivyo Majaliwa ameeleza  namna ambavyo Tume ya kuratibu uthibiti wa dawa za kulevya nchini inavyoendelea na utendaji wake wa kazi ambapo imekamata na kuwatia hatiani watuhumiwa 76 waliokutwa dawa za Viwandani, ambazo ni Heroine na Cocaine.

Moja  ya ajenda katika kikao hicho ilikuwa ni mawaziri ambao ni wajumbe wa Tume hiyo kupokea taarifa ya kazi iliyokwisha fanywa na katika kukabiliana na kukamata kwa dawa za kulevya tangu kuanza kazi kwa tume hiyo.

Ajenda nyingine ni  wizara kutoa  taarifa  na idadi ya watumishi waliohamia Dodoma kwa awamu ya kwanza kati ya watumishi wangapi waliopo kwenye Wizara na kueleza wanadhani Wizara zao kwa mpango waliojiwekea watakamilisha lini kuhamia Dodoma na katika awamu ngapi kati ya awamu sita zilizopangwa.

Mbali na hayo ameitaja nyingine kuwa ni kupokea taarifa ya matumizi ya fedha na miradi ya maendeleo kwa mwezi julai 2016 hadi februari 2017 agenda, ajenda mbayo haitajadiliwa kama mwanzo kwa kila wizara kutoa taarifa ya fedha iliyoingia na kazi zilizofanywa na badala yake watapata taarifa kutoka kwa Waziri wa fedha na kila wizara itakwenda kufanya mapitio na kujiweka vizuri.

Wakati huo huo waziri mkuu ametoa taarifa ya mwenendo wa vita ya dawa za kulevya nchini,ambapo  alisema Tume hiyo ilianza kazi Februari mwaka jana, na katika kipindi cha Julai 2016 hadi Januari 2017 jumla ya watuhumiwa 11503 wamekamatwa kwa kujihusisha na uzalushaji, uuzaji uzambazaji na utumiaji wa dawa hizo.

Majaliwa, amebainisha kuwa, kati ya watuhumiwa hao 11503, watuhumiwa  981i walikutwa na  kesi za kujibu huku 974 wakitiwa hatiani baada ya kubaini kuhusika na makosa hayo.

Katika kikao hicho waziri mkuu amewaagiza mawaziri wote ambao ni wajumbe wa baraza la tume ya kuratibu udhibiti wa dawa ya kulevya nchini kushiriki kikamilifu katika vita hiyo huku akiwakabidhi namba ya kamishina wa dawa za kulevya ili waweze kumpatia taarifa mara wanapokutana na matukio yanayohusiana na dawa za kulevya.

“Taarifa hii imehusisha dawa za viwandani pekee bila kuhusisha bangi na mirungi huku akipongeza mapambano yanayofanywa katika mikoa yote juu ya vita hiyo pamoja na kuwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa mamlaka zote zinazohusika bila woga,”amesema.

Kuhusu pombe haramu na pombe zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki maarufu kama viroba waziri mkuu amesema, msako wa kuondoa bidhaa hizo ambazo zilikuwa zikihatarisha ustawi wa taifa unaendelea.

Amesema katika msako huo walibaini kuwepo kwa kwa makampuni yanayozalisha pombe hizo bila vibali huku wengine wakiweka pombe haramu ya gongo kwenye viroba hivyo.

Katika hatua nyingine waziri mkuu amezungumzia kukamilika kwa mawaziri wote kuhamia Dodoma huku akiwataka kufanyia shughuli zao zote mkoani humo.

Vile vile amesema, awali waliweka utaratibu wa kuhamia Dodoma kwa awamu ambapo  zipo awamu sita na awamu ya kwanza ilikuwa inaanza Agosti 2016 hadi februari mwaka huu ambao ilihusisha mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wote wanaofanya kazi kwa pamoja.

 Na Dotto Kwilasa,Dodoma.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU