Posts

Showing posts from May, 2016

JUBILEI YA WAKLERI YAANZA KUTIMUA VUMBI MJINI VATICAN

Image
Wakleri na majandokasisi kutoka sehemu mbali mbali za dunia kuanzia tarehe 1- 3 Juni 2016 wanaadhimisha Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu kwa kuungana pamoja na Baba Mtakatifu Francisko, ili kumwimbia Mungu utenzi wa sifa na shukrani kwa zawadi na wito wa Daraja Takatifu, mwendelezo wa utume wa Kristo Yesu katika: kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza watu wa Mungu. Kilele cha Jubilei ya Wakleri na Majandokasisi ni hapo tarehe 3 Juni 2016 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kuombea Wakleri Duniani, iliyoanzishwa na Mtakatifu Yohane Paulo II kunako  tarehe 25 machi 1995. Katika barua hii, Mtakatifu Yohane Paulo II kwa namna ya pekee, anatoa kipaumbele cha kwanza kwa utakatifu wa maisha ya wakleri kama chachu muhimu sana kwenye mchakato wa Uinjilishaji mpya unaojikita katika ushuhuda wa maisha. Ulimwengu mamboleo unahitaji wainjilishaji wapya, wenye ari na moyo mkuu, wanaofumbata zawadi ya wito na maisha ya kipadre kama hija inayowaelekeza kwenye utakatif

TUWAPENDE,TUWATHAMINI MAJIRANI ZETU

Image
Kila mwaka ifikapo tarehe 31 Mei, Kanisa linaadhimisha Siku kuu ya Bikira Maria kumtembelea binamu yake Elizabeth sanjari na kufungwa mwezi wa Mei, uliotengwa maalum kwa ajili ya Ibada kwa Bikira Maria Mama wa Mungu na Kanisa. Hii ni Siku kuu ya utenzi wa Bikira Maria unaojikita katika fadhila ya kusikiliza kwa makini, kutafakari na kutenda kwa imani, mapendo na matumaini. Bikira Maria kumtembelea Elizabeth ni tukio la imani, upendo na ambalo linatangaza utimilifu wa nyakati, kwa kuzaliwa Mkombozi wa ulimwengu anayetanguliwa na Yohane Mbatizaji. Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha kilichoko mjini Vatican, katika maadhimisho ya Siku kuu ya Bikira Maria kumtembelea Elizabeth amewataka waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi mema, kujifunza kujisadaka kwa ajili ya huduma ya mapendo kwa ajili ya jirani, jambo ambalo lingeweza kuleta mageuzi makubwa duniani.  Bikira Maria kumtembelea Elizabeth ni tukio linalobubujika furaha i

MAJADILIANO NDIO SULUHU YA MATATIZO YOTE

Image
Vijana wanafunzi mia nne kutoka katika vyuo vikuu zaidi ya arobaini kutoka katika nchi 190 waliokuwa wanashiriki katika kongamano la sita la kimataifa la Taasisi ya Kipapa ya “Scholas Occurrentes” wamehitimisha kogamano hili kwa kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 29 Mei 2016. Lengo lilikuwa ni kuendeleza mchakato wa kubomoa kuta za utengano kati ya watu ili kujenga na kuimarisha madaraja ya kuwakutanisha watu yanayojikita kwa namna ya pekee katika elimu mashuleni. Kongamano limewashirikisha wadau kutoka katika sekta ya mawasiliano ya jamii; sanaa na michezo; sayansi na teknolojia. Kauli mbiu ya maadhimisho haya ilikuwa ni “Chuo kikuu na shule: ni ukuta au daraja?” . Hii ilikuwa ni fursa muafaka kwa washiriki wa kongamano hili kuweza kupembua kwa kina na mapana dhana ya taasisi za elimu ya juu na shule mintarafu mwono wa Baba Mtakatifu Francisko, dhana aliyoifanyia kazi takribani miaka kumi na mitano iliyopita. Baba Mtakatifu Fran

MAGAZETI LEO JUMANNE HAYA HAPA

Image

TABATA WASHEREHEKEA EKARISTI TAKATIFU

Image
  Waamini wa Parokia ya Kristo Mfalme Tabata Jimbo kuu Katoliki Dar es Salaam wamesherehea sikukuu ya Ekaristi Takatifu kwa maandamano na shamrashamra zingine za kuvutia.Pata picha kadhaa za tukio hilo kama lilivyoshuhudiwa na BLOG yako pendwa.

SHEREHE YA EKARISTI TAKATIFU-MAANA HALISI NI MAANDAMANO

Image
Sherehe ya   Ekaristi Takatifu – maana halisi ni maandamano Tunaadhimisha Sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo kila mwaka siku ya Alhamisi inayofuata baada ya kuadhimisha Sherehe ya Utatu Mtakatifu. Kwa kuwa Sherehe hiyo ni   Sikukuu ya amri, Kanisa imeruhusu kuiadhimisha   siku ya Dominika inayofuata ili   Wakristo wote waweze kutimiza wajibu wao wa kusali .   Kuanza na Kuenea   Kihistoria Sherehe hiyo ilianza huko Ufaransa kutokana na maono ya mtawa Juliana aliyoanza kuyapata mnamo mwaka 1209. Baada ya juhudi kubwa ya kumwomba Askofu wake kuanzisha Sherehe hiyo, hatimaye   ombi la sista Juliana lilipokelwa. Mwaka 1246 iliadhimishwa kwa mara ya kwanza huko Lie’ge   nchini Ufaransa. Mwaka 1264 Papa Urban IV (wa nne) aliitangaza Sherehe hiyo iadhimishwe popote katika Kanisa. Kumbe kabla ya kuteuliwa kuwa Papa,   Urban alikuwa shemasi na baadaye padri wa jimbo hilo la Liege, alishaifahamu historia ya sikukuu hiyo.   Papa Urban IV alimwomba

JUBILEI YA MASHEMASI

Image
Mashemasi ni watumishi na mitume wa Kristo wanaotumwa kumtangaza na kumshuhudia Yesu kwa njia ya huduma ya mapendo. Yesu Kristo amejifunua kama Neno wa Baba ambaye amekuja kuwatangazia watu Habari Njema ya Wokovu, akawa ni chemchemi ya furaha na huduma kwa wote, yaani akawa Shemasi. Hii ndiyo changamoto inayotolewa kwa watangazaji na wahudumu wa Habari Njema ya Wokovu kuhakikisha kwamba, wanafuata kikamilifu maagizo ya Kristo Yesu. Ikumbukwe kwamba, dhamana ya Uinjilishaji ni kwa Wakristo wote na huduma ya upendo ni njia muafaka ya kumwilisha utume wa kumfuasa Yesu, kielelezo cha ushuhuda wa maisha yanayojikita katika huduma. Hii ni sehemu ya mahubiri yaliyotolewa na Baba Mtakatifu Francisko wakati wa maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu kwa Mashemasi wa kudumu, Jumapili tarehe 29 Mei 2016. Ili kuwa kweli ni watumishi wema na waamifu, kuna haja ya kujikita katika dhana ya uwepo, tayari kujisadaka bila ya

SIKU YA MTOTO DUNIANI JUNI MOSI,PAPA ATOA WITO

Image
Baba Mtakatifu Francisko baada ya kuadhimisha Ibada ya Misa takatifu kwa ajili ya kuhitimisha maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu kwa Mashemasi wa kudumu, Jumapili tarehe 29 Mei 2016, amewashukuru na kuwapongeza Mashemasi wote waliohudhuria kutoka ndani na nje ya Italia kwa uwepo wao ndani ya Kanisa. Baba Mtakatifu pia ametumia nafasi hii kuwasalimia mahujaji kutoka sehemu mbali mbali za dunia waliohudhuria tukio hili la kihistoria, wakati huu wa maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu. Baba Mtakatifu amewashukuru kwa namna ya pekee washiriki wa kongamano na hija ya msamaha lililoandaliwa na Chama cha kitume cha Celestino; Chama cha Kitaifa cha utunzaji wa nishati rafiki, kinachoendelea kutoa elimu juu ya utunzaji bora wa mazingira bila kuwasahamu mahujaji kutoka Poland ambao, siku ya Jumapili, wamefanya hija kwenye Madhabahu ya Bikira Maria Piekary. Baba Mtakatifu anamwomba Bikira Maria, Mama wa huruma kuzitegemeza fami

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 30

Image