Posts

Showing posts from October, 2017

UGONJWA WA MARBURG NCHINI: TAHADHARI YATOLEWA

Image
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), mnamo tarehe 19 Oktoba 2017 kuhusu ugonjwa wa Marburg ambao umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda tangu tarehe 17 Octoba, 2017. Maeneo yaliyoathirika  na ugonjwa huo ni Wilaya ya Kween, Kanda ya Mashariki ya nchi, ambayo  inapakana n nchi ya  Kenya. Hadi kufikia  tarehe 19 Oktoba 2017, watu 4 walikwishapata maambukizo ya ugonjwa huo, ambapo wawili kati yao   wamepoteza maisha. Wizara  inatoa tahadhari ya Ugonjwa huu kwa wananchi  katika mikoa yote ya Tanzania, hususan kwa wale wanaoishi  katika mikoa ambayo inapakana na na nchi  ya Uganda (Mikoa ya Mara, Mwanza na Kagera). Ugonjwa wa Marburg  unafanana sana na ugonjwa wa Ebola. Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Marburg vinajulikana kama  “Marburg Virus”, navyo vipo katika jamii moja na virusi vinavyosababisha Ebola (Ebola virus). Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yajulikanayo kwa uju

RATIBA YA BABA MTAKATIFU MWISHONI MWA MWAKA HUU 2017

Image
Ziara ya Kitume nchini Chile na Peru kuanzia tarehe 15 -22 Januari 2018, Misa ya tarehe 2 Novemba katika Makaburi ya waamerika Nettuno na Siku ya Masikini  Duniani  tarehe 19 Novemba katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Ni baadhi ya matukio katika ratiba ya Baba Mtakatifu Francisko iliyotolewa mapema karibuni kwa miezi kuanzia Novemba, Disemba 2017 na Januari 2018 iliyothibitisha katika Kalenda ya maadhimisho ya Baba Mtakatifu ktuoka katika Ofisi ya Maadhimisho ya Liturujia Vatican. Baba Mtakatifu ataadhimisha misa ya kumbukumbu ya waamini marehemu huko Nettuno Italia tarehe 2 Novemba 2017, baadaye, tarehe 3 Novemba ataadhimisha misa nyingine katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa ajili ya kukumbuka makardinali na maaskofu marehemu waliofariki kwa kipindi cha mwaka huu. Tarehe 19 Novemba anatarajiwa kuadhimisha misa Takatifu kwa ajili ya Siku ya Maskini Duniani, aliyoitangaza mwishoni wa mwaka wa Jubilei ya huruma, na wiki itakayofuata kuanzia tarehe 26 Novemba ha

UFUNGUZI MWAKA WA MASOMO 2017/2018 CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AGUSTINO (SAUT) MWANZA

Image
 Matukio mbalimbali ya Misa ya ufunguzi wa mwaka wa masomo 2017/2018 Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) Mwanza katika ukumbi wa m9. Adhimisho hilo limeongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Padri Tadeus Mkamwa. Picha na George Alexander...Habari zaidi soma gazeti KIONGOZI juma hili.

STENDI KUU WAANZISHA JUMUIYA, WAWA MFANO KWA WENGINE

Image
WAKRISTO wanaofanya kazi katika maeneo ya stendi kubwa nchini wameshauriwa  kuanzisha umoja wa jumuiya ndogondogo katika maeneo yao ya kazi ili kushiriki masuala ya ibada na taratibu za Kanisa kwakuwa wengi wao hawashiriki kusali jumuiya katika makazi yao kwani muda mwingi wanautumia katika mazingira yao ya kazi. Wito huu umetolewa na wanajumuiya ya “ watakatifu wote” wafanyao kazi katika maeneo ya Stendi Kuu jimboni Sumbawanga hivi karibuni wakati wa maandamano ya matembezi ya msalaba wa Jubilei ya miaka 50 ya parokia ya Kanisa Kuu jimboni humo ambapo maandamano hayo ya kutembeza msalaba yaliuteka mji wa Sumbawanga  kuanzia maeneo ya stendi kubwa ya mabasi iliyopo Sokomatola na kuhitimishwa katika parokia ya Kanisa Kuu na kupokelewa na Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga Mhashamu Damian Kyaruzi. Akizungumza kwa niaba ya wanajumuiya ya Watakatifu Wote, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Ernesti Kasanka amesema kuwa tangu alfajiri hadi jioni wanashinda stendi, kwa maana hiyo

ZIGO LAKO USIMTWISHE MTU, PAMBANA NALO MWENYEWE

Image
Binadamu tuna hulka ya kuwatwisha watu zigo la lawama pindi tunapoonekana tumeshindwa kutimiza malengo au wajibu wetu iwe nyumbani ama katika jamii zinazotuzunguka. Mifano ipo mingi. Baba katika familia ameshindwa kutimiza majukumu yake kama baba kwa mama; kumtunza, kumjali, kumheshimu, kumvumilia, kutosaliti ndoa na zaidi kumpenda kwa dhati. Matokeo yake mama kaona hayo hayapati kaanza naye kupoteza sifa za “umama” ndani ya nyumba. Mzee kaanza mara ooh dada zake wanamrubuni, ooh mashoga zake wanamhadaa, ooh wazazi wake ndio chanzo, ooh kapata mtu mwingine nje ya ndoa n.k. Kijana hasomi, hajibidiishi, hana machungu na ada na gharama wazazi au walezi wake wanazotoa ili afaulu vizuri masomo yake. Kutwa yupo mitandaoni akichati hili na lile, anajiingiza katika mahusiano akiwa mdogo, anajihusisha na matumizi ya dawa za kulevya, unywaji viroba, mwisho wa siku anapofeli utasikia aah dingi mnoko, maza anabana, ticha ananifuatilia sana. Kabla hajapata ajira na baada ya kutes

PAROKIA MPYA YAZINDULIWA JIMBO KUU KATOLIKI DODOMA

Image
KATIKA   safari   ya   kueneza    Injili   kwa   watu   wote   hapa   duniani, Jimbo   Kuu   Katoliki Dodoma   limepata   Parokia   mpya   ya   Pwaga   iliyozinduliwa   hivi   karibuni   na   Askofu   Mkuu   wa Jimbo   hilo Mhashamu     Beatus   Kinyaiya OFM-Capp. Akizindua parokia   hiyo   mpya hivi karibuni, Askofu   Mkuu Kinyaiya OFM-Capp amesema   kuwa   safari   ya   injili   ni ngumu   na   kuwa   si   vyema   wanadamu    kuipuuzia    kwani   ni   safari   ya   toba huku Kanisa   likiwa ni   moyo   wa   muamini   popote   pale na   kuwa   pamoja   na   kuwa   parokia   hiyo   mpya   haina   jengo   kubwa lakini Kanisa   ni   watu   na ni   popote   pale bila kujali   ni   wapi   wanasalia, la msingi ni kuwa   na   imani   kwa   Mungu. “Mama    Kanisa    anasisitiza   watu     kusali   kwa   moyo   na   nguvu   kubwa    bila   kujali   sala    inafanyika   wapi, mkristo   anatakiwa kusalia   mahali   popote    kwani   sala   ni   Baraka   na muamini   anapat

Maaskofu Katoliki wataka hukumu ya kifo itazamwe upya

Image
MAASKOFU wa Kanisa Katoliki nchini wameiasa serikali kubadili sheria inayoruhusu adhabu ya kifo kwa wahalifu badala yake watoe hukumu ya kifungo cha maisha. Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya ameeleza hayo kwa niaba ya Maaskofu Katoliki Tanzania hivi karibuni huko jimboni TUNDURU-Masasi kwenye ibada ya mazishi ya Askofu wa Jimbo hilo marehemu Castory Msemwa. “Leo tunapomzika Askofu Msemwa tunakumbuka kuwa mwanadamu anazaliwa na anakufa kupitia vifo mbalimbali ukiwemo uzee na magonjwa. Huo ni mpango wa Mungu kwamba mwanadamu afe ili afike kwenye makao aliyomuandalia. Lakini kuna vifo ambavyo ni kinyume na mpango wa Mungu ikiwemo sheria inayoruhusu mahakimu kutoa hukumu ya kifo. Aliye na mamlaka ya kuchukua uhai wa mwanadamu ni Mungu peke yake kwani uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu. Sababu ya vifo vinavyotokea duniani ni sisi wanadamu wenyewe. Maandiko matakatifu yanatuambia Mungu peke yake ndiye ana uwezo na mam