UGONJWA WA MARBURG NCHINI: TAHADHARI YATOLEWA

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), mnamo tarehe 19 Oktoba 2017 kuhusu ugonjwa wa Marburg ambao umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda tangu tarehe 17 Octoba, 2017. Maeneo yaliyoathirika  na ugonjwa huo ni Wilaya ya Kween, Kanda ya Mashariki ya nchi, ambayo  inapakana n nchi ya  Kenya. Hadi kufikia  tarehe 19 Oktoba 2017, watu 4 walikwishapata maambukizo ya ugonjwa huo, ambapo wawili kati yao   wamepoteza maisha.

Wizara  inatoa tahadhari ya Ugonjwa huu kwa wananchi  katika mikoa yote ya Tanzania, hususan kwa wale wanaoishi  katika mikoa ambayo inapakana na na nchi  ya Uganda (Mikoa ya Mara, Mwanza na Kagera).

Ugonjwa wa Marburg  unafanana sana na ugonjwa wa Ebola. Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Marburg vinajulikana kama  “Marburg Virus”, navyo vipo katika jamii moja na virusi vinavyosababisha Ebola (Ebola virus). Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yajulikanayo kwa ujumla kama Homa za Virusi zinazosababisha kutokwa damu mwilini, (Viral Haemorrhagic Fevers). Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo.

Dalili kuu za ugonjwa huu ambazo huanza ghafla ni pamoja na Homa kali, maumivu makali ya kichwa pamoja na mwili kuishiwa nguvu ambapo baadaye huambatana na kuharisha sana (majimaji), maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika na kutokwa damu katika matundu yote ya mwili yaani pua, njia ya haja kubwa na ndogo, mdomoni, masikioni, machoni, hali inayopelekea kifo kwa muda mfupi. Kipindi cha kuonekana kwa dalili za ugonjwa ni kati ya siku 3 hadi 9 baada ya kupata maambukizi.

Ugonjwa huu unaenea kwa urahisi sana na ha­raka kutoka mtu mmoja hadi mtu mwingine iwapo mtu atakuwa karibu na mgonjwa na kugusana na mate, damu, mkojo, machozi, kamasi, maji maji mengine ya mwili, ikiwa ni pamoja na jasho au kumgusa  mtu aliyekufa kwa ugonjwa wa Marburg. Ugonjwa huu pia unaweza kuenezwa iwapo mtu atagusa nguo au mashuka ya mgonjwa wa Marburg.

Wizara ya Afya , imechukua hatua zifuatazo katika kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:

Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kupitia OR-TAMISEMI. Taarifa hiyo imejumuisha namna  Ukweli kuhusu ugonjwa (Fact sheet),

Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipaka ya nchi kavu na maji. Aidha watalaamu hawa wa Afya pia wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu dalili za ugonjwa huu ili endapo ugonjwa huo utatokea uweze kutolewa taarifa mapema na kushughulikiwa.

Vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya na vipima joto maalum (thermoscan) tayari vipo katika maeneo husika ya mikoa.

Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani hadi  sasa hakuna mgonjwa yeyote wa Marburg aliyeripotiwa nchini. Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa kuwa na dalili za ugonjwa huu.

Kitengo cha mawasiliano ya Serikali


Comments

  1. I want every herpes patient to please read my testimony, my name is SARAH MORGAN am from California in USA, I contacted genital herpes from my ex boyfriend who never had any symptoms. I have had it for 4 months now., and it has affected my life. I have told my boyfriends who I trusted about it and I have never had a bad reaction, it has affected my new relationships with Smith and people think herpes is really a minor skin irritation herpes has a long term effects on health. The stigma attached to this virus by ignorant people is ridiculous. Most people have herpes in one form or another. I would like to advise people on how I get rid of my herpes and I was reading a comment on the internet,and I saw a testimony posted by a woman from Germany that she get rid of her herpes with the help of DR AHKIGBE and so I was so happy when I saw that post, that his herbal medication is free and I quickly collected the herbal doctor email and I email him within 3 hr he respond to my email and I explain things to him he told me not to worry that he is going to cure me totally with his herbal medicine he only request for little money that he will use to buy the items for the preparation of the herbal medicine, wish I send to him because the pain was too much for me to bear and after some days he told me that he has prepare the herbal medicine, that I should send him my address that he want to sent it to me via DHL or FED-EX that was how I got the herbal medication and I use it as I was told and after few days I found out that my herpes was no more, i went to hospital for confirmation and it was true really that was how i got my cured. DR AKHIGBE also cure other deadly diseases like,  HIV/AIDS, HERPES, DIABETES,CANCER, ALS, ASTHMA, HERPAPITIS A&B, DENGUE FEVER, RABIES, MARBURG DISEAS, THYROID, MENINGITIS ,LUPUS, EPILEPSY, CHRONIC DISEASE, MALARIA, BACTERIAL DIARRHEA HEART DISEASE., JOINT PAIN, STOMACH PAIN, SCHIZOPHRENIA, POLIO,MULTIPLES SCLEROSIS, HIGH BLOOD PRESURE, TUBERCULOSIS, ALZHEIMER , PENIS ENLARGEMENT, PARKINSON'S, to get your rid kindly via his email:   drrealakhigbe@gmail.com    contact his number:  +2349010754824           website:  https://drrealakhigbe.weebly.com       you can still write me on Instagram to get more information. on Sarah Morgan.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU