Posts

Showing posts from September, 2017

MAPADRI WENYE TAMAA WAONYWA

Image
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mhashamu Paulo Ruzoka amewaasa mapadri kukaa chonjo na mali za ulimwengu huu unaopita ili wasiingie matatani na kuipoteza imani yao safi. Rai hiyo ameitoa hivi karibuni katika adhimisho la Misa Takatifu na kutoa Sakramenti ya Daraja Takatifu ya Upadri kwa Shemasi Peter Fabian Kulwa hivi karibuni. Akitoa mahubiri yake katika Kanisa la Mtakatifu Yosefu Mfanyakazi Kipalapala Tabora, Askofu Mkuu Ruzoka amewataka mapadri kupeleka upendo wa Kristo kwa watu wote bila ya ubaguzi wowote. Amesema Mtakatifu Matayo mtume na mwinjili alikubali kuacha kazi yake nzuri ya mshahara akakubali kumfuata Kristo, vivyo hivyo na padri anapoitwa hana budi kuacha yale yote yasiyoendana na wito mtakatifu wa upadri na kumsikiliza Kristo anachomtaka akifanye kwa watu wake. Pia Askofu Mkuu Ruzoka amesema wito wa upadri ni zawadi toka kwa Baba Mungu ambayo padri anazawadiwa bila mastahili yake mwenyewe. Na kama mtu atasema nataka kuwa padri bila kuitwa n

CRS YAWARAHISISHIA HUDUMA YA MAJI WAKAZI KARATU

Image
SHIRIKA la Catholic Relief Services (CRS) kwa kushirikiana na  mdau wake Grundfos Lifelink  A/S kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii Jimbo Katoliki Mbulu (DMDD) limebuni mradi wa kipekee na wa kwanza nchini Tanzania unaolenga kubadilisha mfumo wa  kulipia maji kutoka malipo ya baada kwa sasa na kuja kwenye malipo ya kabla kwa kutumia vocha katika utoaji wa huduma ya maji. Kwa mujibu wa Meneja mradi kutoka CRS Mhandisi Ephraim Tonya, mradi huo unalenga kuhudumia watu zaidi ya 11,604 kwa awamu ya kwanza kutoka wilaya ya Karatu mkoani Arusha ulioanzia katika kijiji (1)  cha Gongali na mitaa minne (4) Karatu mjini ambayo ni Mjini kati, Bomani, Mazingira bora na Sabato vinavyohudumiwa na bodi ya  KAVIWASU na kijiji cha Qaru kinachohudumiwa na bodi ya ENDAWASU. Mhandisi Tonya ameeleza kuwa lengo la mradi huo wa kulipa maji kabla ni kuwezesha  udumisho na uendelevu wa miradi ya maji, upatikanaji wa huduma muda wote mtumiaji anapohitaji, kuongeza ufanisi katika ufanyaji k

KANISA KATOLIKI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI

Image
IDARA ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) imefanya mkutano wa Mwaka ili kutathmini utendaji kazi pamoja na kujadili mbinu za kuboresha utoaji huduma za Afya katika hospitali na vituo vya Afya vinavyomilikiwa na Kanisa Katoliki nchini. Mkutano huo umefanyia hivi karibuni katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Kurasini jijini Dar es Salaam ukijumuisha Makatibu wa Afya Jimbo, madaktari wa hospitali zinazomilikiwa na   Kanisa Katoliki, wasimamizi na Wakuu wa Vituo vya Afya vya Kanisa Katoliki. Akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa Kamati ya Afya TEC Askofu Mkuu Jude Thadeus Ruwaich amesema kuwa anatumaini mkutano huo utaleta matokeo yenye tija katika kuboresha utoaji wa huduma ya afya kwa hospitali na vituo vya afya chini ya Kanisa Katoliki kwa wananchi. Ajenda kuu ya mkutano huo ni "Kuimarisha uwezo wa Vifaa vya Afya katika hospitali na vituo vya Afya vya Kanisa Katoliki kutoa huduma   bora: Kutathmini uwezo, fursa, udhaifu, changamoto na kua

MAGUFULI SAFI, ILA ATUPE KATIBA MPYA-ASKOFU NIWEMUGIZI

Image
ASKOFU Severine Niwemugizi wa Jimbo Katoliki Rulenge Ngara amesema anaridhishwa na utendaji kazi wa Rais John Magufuli kwa nia yake ya kuleta maendeleo nchini, lakini anamuasa aangalie vipaumbele vya wananchi ikiwemo kuwa na Katiba Mpya. Akizungumza na Gazeti Kiongozi baada ya kumaliza Mkutano wa zaidi ya asasi 80 za Kiraia wa kufufua mchakato wa katiba uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Askofu Niwemugizi amesema kuwa, ni wazi Rais John Magufuli anapambana na ufisadi kwa ajili ya kulinda rasilimali za nchi, anahamasisha wananchi kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi lakini atafanikiwa endapo atakuwa na Katiba ambayo ndiyo dira ya nchi. “Ile tathmini ya mwaka mmoja wa utendaji kazi wa Rais Magufuli ni wazi ilionesha kazi alizozifanya na mafanikio na wananchi tuliridhika tukaona kuwa kweli tumepata Rais. Kazi ya kupambana na rushwa, maadili kwa viongozi wa umma na amengine mengi, lakini ili aweze kuyaendeleza awe na katiba madhubuti. Aangalie maoni ya wananchi kup

MAGAZETINI LEO IJUMAA TAREHE 29 SEPTEMBA

Image