Posts

Showing posts from February, 2017

Ujumbe wa Papa Francisko kwa Kipindi cha Kwaresima 2017

Image
Baba Mtakatifu Francisko anasema, maskini wanaolala mlangoni pa matajiri si kero inayopaswa kushughulikiwa kama “chuma chakavu” bali ni mwaliko wa kutubu na kumwongokea Mungu sanjari na kubadili mfumo wa maisha tayari kuwakumbatia na kuwasaidia wengine katika shida na mahangaiko yao. Changamoto kubwa wakati wa Kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2017 ni kujitahidi kumwilisha sehemu ya Injili la Lazaro maskini na tajiri asiyejali wala kuguswa na mahangaiko ya jirani zake. “Neno ni zawadi; jirani yako ni zawadi pia”. Hii ndiyo kauli mbiu inayoongoza ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko katika kipindi cha Kwaresima kwa Mwaka 2017, muda wa kusali, kutafakari, kujikita katika maisha ya Kisakramenti, lakini zaidi kumwilisha matendo ya huruma kiroho na kimwili kama kielelezo cha imani tendaji! Baba Mtakatifu anasema, Kipindi cha Kwaresima ni mwanzo mpya na njia inayowaelekeza waamini katika maadhimisho ya Siku kuu ya Pasaka, kielelezo cha ushindi wa Kristo Yesu dhidi ya dhambi na mauti, muda w

MAGAZETINI LEO JUMANNE FEB 28

Image

MAGAZETINI LEO JUMATATU FEB 27

Image

“Simamieni ukweli” Askofu Kimaryo awaasa mapadri

Image
MAPADRI wametakiwa kuwa wakweli katika kila jambo watendalo ili kuwakomboa wanyonge na wahitaji kutoka katika hali mbaya kimaisha na kiroho. Askofu wa Jimbo Katoliki Same Mhashamu Rogarth Kimaryo ametoa rai hiyo katika Misa Takatifu ya uzinduzi wa Jubilei ya miaka 100 ya upadri Tanzania Bara katika Jimbo hilo. “Mapadri lazima muuige mfano wa Nabii Yeremia aliyeitwa na Mwenyezi Mungu na kupewa majukumu yaliyomfanya akabiliane na wafalme, wakuu, makuhani na watu wa mamlaka akitetea ukweli hata kutaka kukatwa kichwa, lakini alisimamia alichotumwa na Mwenyezi Mungu na kukitimiza,” amesema Askofu Kimaryo Amesema mapadri wametumwa na Mungu ili kuutumikia wito kwa kuwatetea wanyonge na kujitenga na faida na tamaa za kidunia ambazo zitawaingiza katika matatizo makubwa, hivyo wanatakiwa kuyaishi mafunzo ya Kanisa tu. “Hapa duniani mmeteuliwa kuwasaidia wahitaji tu kiroho, siyo kuzitumia elimu zenu kubwa na talanta kujitajirisha, hayo mngeyapata kirahisi nje ya wito wa kipadri, mkiyaz