Wanaokimbilia miujiza ya uponyaji watahadharishwa

WITO umetolewa kwa waamini nchini kuacha kutafuta uponyaji wa magonjwa yao kwa njia za mkato badala yake wajiaminishe kwa Mungu na kwenda sehemu sahihi ya kupata huduma za tiba.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza Mhashamu Yuda Thadei Ruwaichi, katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya Wagonjwa duniani, iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza.
Askofu Ruwaichi amewataka baadhi ya waamini wanaokimbilia uponyaji kwa miujiza kujitafakari na kufanya maamuzi sahihi kwa kuiga mfano wa Kristo ambaye katika magumu yote aliruhusu mapenzi ya Mungu yatimizwe.
“Nimeona matangazo mengi yanayowaalika watu waende kuponywa kwa miujiza, na pia huko mnakimbilia wengi. Najua huwa mnaenda wengi. Hebu mjikusanye vizuri, mtafakari na mfanye lile lililo sahihi” ameeleza Askofu Ruwaichi. 
Aidha ametoa wito kwa waganga, wauguzi na wote wanaohusika kuwahudumia wagonjwa kujenga utayari na moyo wa kusikiliza kwa dhati, kwa kuwa wagonjwa wengi, hasa wale wanaokimbilia kutafuta majibu pasipo na majibu, wanaenda mahali wanapoamini wanasikilizwa.
“Siyo kusikiliza kama mtu aliyekereka, bali kusikiliza kama mtu ambaye anatimiza wito mtakatifu aliojaliwa na Mungu wa kulinda na kusaidia uhai wa binadamu ustawi na kuendelea” ameongeza.
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa magonjwa ya Saratani katika Hospitali ya Rufaa Bugando, Dk. Nestory Masalu ameeleza kuwa kukithiri kwa magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza kunasababishwa na tabia ya watu wengi kukimbilia tiba mbadala ambazo husababisha kuacha kutumia dawa walizoshauriwa kutumia.
Akitoa mada katika siku hiyo ya wagonjwa duniani ambayo kitaifa imefanyika Jimbo kuu Katoliki Mwanza, Dk. Masalu amesema kuwa kutokuwa na desturi ya kupima afya husababisha mgonjwa kutumia dawa nyingi pale ugonjwa unapogundulika.
“Kumekuwa na uelewa mdogo wa magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza. Watu wengi wamekuwa wanatumia gharama kubwa kwa tiba mbadala, wakiwa na imani au kuaminishwa kwamba watapona, na hivyo kuacha dawa za hospitali. Matokeo yake hao wagonjwa huja na hali mbaya sana hospitali na wakati mwingine inakuwa ngumu kutibika” ameeleza.
Aidha katika kukabiliana na magonjwa sugu yasiyoambukizwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa kushirikiana na Idara ya Tiba imeweka mipango ya muda mrefu ya kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni pamoja na kuadhimisha siku za magonjwa husika kama figo, sukari na moyo na shinikizo la damu, ambapo hufanya uchunguzi wa bure na kutoa ushauri kwa magonjwa husika.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amelishukuru  Kanisa Katoliki kwa kutenga fursa ya kuwakumbuka na kuwaombea wagonjwa, kwani daima limekuwa mdau mkubwa katika sekta ya afya.
Aidha Mongela ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, ametoa rai kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kufanya mazoezi ili waweze kuimarisha afya zao na kujikinga na maradhi mbalimbali.

Jimbo Kuu la Mwanza kuadhimisha siku ya wagonjwa kila mwezi

Katika hatua nyingine Askofu Ruwaichi ameziagiza parokia zote za Jimbo Kuu Katoliki Mwanza

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU