Posts

Showing posts from April, 2016

Papa amteua Padri Kassala kuwa Askofu mpya Jimbo la Geita

Image
Baba Mtakatifu Fransisko amemteua Padri Flavian Kassala kuwa askofu mpya wa Jimbo Katoliki Geita. Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padri Raymond Saba kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Askofu Mkuu Fransisko Padilla anayo furaha kutangaza kuwa Papa Fransisko amemteua Padri Kassala kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Geita. Mpaka wakati wa uteuzi wake Askofu mteule Kassala alikuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Maris Mtwara. Askofu mteule Kassala amezaliwa Desemba 4, 1967 katika Parokia ya Sumve, Jimbo Kuu Katoliki Mwanza. Alipata masomo yake ya Sekondari katika Seminari ndogo ya Mtakatifu Pio wa X, iliyoko Makoko, Jimbo Katoliki la Musoma. Alijiendeleza zaidi kwenye Seminari Ndogo ya Sanu Jimbo Katoliki Mbulu. Masomo ya falsafa aliyapata kutoka Seminari ya Mtakatifu Anthony wa Padua- Ntungamo, iliyoko Jimbo Katoliki la Bukoba. Askofu mteule Kassala alijipatia elimu ya Teoloji

TANZANIA INTERFAITH PARTNERSHIP KUUTOKOMEZA UKIMWI

Image
Tanzania Interfaith Partnership(TIP) shirika linalojumuisha taasisi za dini Tanzania yaani Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Jumuiya ya Kikristu Tanzania (CCT), Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), na Ofisi ya Mufti Zanzibar (MOZ) limefanya kikao huku lengo kubwa likiwa ni kuweka mkakati wa pamoja wa kupambana na ugonjwa wa ukimwi,kuboresha maelewano baina ya dini zote,kuboresha amani na mshikamano uliopo nchini. Taasisi hizi zilianza kushirikiana mwaka 2002 chini ya   Balma in Gilead ambalo ni Shirika la Kimarekani. Pamoja na mambo mengine,kikao hiki kimejadili namna ya kutoa huduma za afya hasa za kupambana na Maambukizi ya UKIMWI na UKIMWi wenyewe . Mkakati huu unaohusisha mikoa ya Kigoma, Manyara na Mara unalenga zaidi,watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi,huduma za wagonjwa nyumbani, ushauri nasaha na upimaji VVU kwa hiari, na kinga dhidi ya UKIMWI.   Kikao hiki kimehudhuriwa na wakuu wote wa taasisi za dini kama ifuatavyo: Askofu Tarcisius Ng

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI YAMEANDIKA HIKI..

Image

PENYE WAWILI KUNA JAMBO...

Image
Baba Askofu wa Jimbo Musoma Michael Msonganzila akiteta jambo na Baba Askofu wa Jimbo Kondoa Bernadin Mfumbusa hivi karibuni mjini Dodoma katika mazishi ya Askofu mstaafu Mhashamu Mathias Isuja.(Picha na Bernard James).

SOMO KWA WAFUNGWA

Image
Baba Mtakatifu Francisko amewashukuru na kuwapongeza wafungwa wanaotumikia adhabu yao huko Velletri, Italia kwa kumwandikia barua inayoonesha shida, mateso na mahangaiko yao ya ndani na kwamba, anawakumbuka na wakati mwingine hata yeye mwenyewe anatafakari kuhusu hali ya gereza katika maisha yake. Kutokana na changamoto hii, ndiyo maana wakati wa hija zake za kitume anapenda kukutana na kuzungumza na wafungwa Gerezani, ili kuwaonesha upendo na uwepo wake wa karibu katika shida na mahangaiko yao! Baba Mtakatifu anaendelea kusema, katika maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, kutakuwepo na siku moja kwa ajili ya Jubilei ya wafungwa, siku ambayo Kanisa litashikamana kwa pamoja kwa ajili ya kusali na kuwaombea wafungwa magerezani, kielelezo cha uwepo wa karibu kiroho! Baba Mtakatifu anawaambia wafungwa kutoka kata tamaa, bali waendelee kuwa na matumaini hata pake wanapodhani kwamba, muda kwao umesimama na wala hausongi mbele! Baba Mtakatifu an

HUDUMA KWA WATU WA MUNGU YASISITIZWA

Image
Hivi karibuni Tume ya Kipapa ya Amerika ya Kusini ilifanya mkutano wake wa mwaka kwa kuongozwa na kauli mbiu “Umuhimu wa waamini walei katika maisha ya hadhara katika nchi za Amerika ya Kusini”. Wajumbe hawa wakapata nafasi ya kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko mjini Vatican aliyewataka viongozi wa Kanisa kuhudumia vyema familia ya Mungu kwa kuwaangalia, kuwalinda, kuwasindikiza, kuwaenzi na kuwahudumia kwa kutambua kwamba, viongozi wa Kanisa ni wachungaji wa Kondoo wa Kristo wanaopaswa kuandamana nao katika hija ya maisha! Baba Mtakatifu katika barua aliyomwandikia Kardinali Marc Armand Ouellet, Rais wa Tume ya Kipapa ya Amerika ya Kusini anawaalika kwa namna ya pekee viongozi wa Kanisa kuwaangalia watu wa Mungu na kujisikia kuwa ni sehemu muhimu sana ya maisha yao ili kusaidia mchakato wa kuenzi maisha na utume wa waamini hawa kwa kutambua kwamba, huu ni wakati muafaka kwa waamini walei kushika hatamu katika maisha na utume wa Kanisa! Lakini kwa ba

UJUMBE WA MEI MOSI

Image
Baraza la Maaskofu Katoliki Canada katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani inayoadhimishwa Mei, Mosi, 2016 linawataka wadau mbali mbali katika ulimwengu wa wafanyakazi kusimama kidete kulinda, kutetea na kudumisha utu na heshima ya binadamu hasa wakati huu kutokana na maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia. Maaskofu katika waraka wao unaoongozwa na kauli mbiu “Kanisa na Jamii” wanagusia kwa namna ya pekee masuala ya haki jamii, haki msingi za binadamu pamoja na athari zinazoendelea kujitokeza katika ulimwengu wa wafanyakazi kutokana na maendeleo makubwa ya sayansi ya teknolojia katika shughuli za uzalishaji na huduma za kijamii! Yanagusa: fursa za ajira, mafao ya wengi, ugawaji wa rasilimali na mafungamano ya kijamii. Mwelekeo wa maendeleo ya teknolojia unaonesha kwamba, baada ya muda si mrefu kazi nyingi ambazo zilikuwa zinatendwa na wafanyakazi, zitaanza kutekelezwa na mashine, hali ambayo italeta mageuzi makubwa katika mchakato mzima wa mtindo wa

JISOMEE MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 27 HAPA..

Image

MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 26..YASOME

Image