MUHIMU SANA



JE UNALIJUA SHIRIKA LA MASISTA WA UPENDO?

Shirika hili lilianzishwa mwaka 1950,mwanziilishi wa shirika hili ni Mwenyeheri mama Terezia wa Calcutta.Shirika hili linaongozwa na karama ya Bwana wetu Yesu Kristo pale msalabani.Pia kufanya kazi kwa ajili ya ukombozi wa Roho za watu.
Shirika hili linaongozwa na karama ya watu ya kukidhi kiu ya milele ya Bwana wetu Yesu Kristo pale msalabani.Pia kufanya kazi kwa ajili ya ukombozi wa Roho za watu.
Shirika hili limesambaa sana Duniani, masista hawa wanafanya kazi katika mabara na nchi zifuatazo:India,Amerika yote ya kaskazini,Amerika ya kati,Amerika ya kusini,Mashariki ya kati, Afrika ya kaskazini,Afrika Magharibi,Afrika ya kati,Afrika ya kusini,Misri,Libya,Morocco, Algeria,Tunisia,Sudani,Djibuti,Uhabeshi,Kenya,Tanzania,SieraLeone,Liberia,Kameruni,Benini,Nigeria,Gambia,Burkina Faso na Mali.
Masista pia wapo katika nchi ya Afrika, Uganda, Burundi, Rwanda, Chad, Afrika kusini, Msumbiji, Congo , Kongo (DRC), Malawi, Niger, Ivory Coast, Zimbabwe, Zambia, Mauritius, Visiwa vya Ushelisheli, Madagascar.
Tuone pia katika bara la Ulaya.
Masista wanafanya kazi katika nchi za Uingereza, Ireland, Iceland, Denmark, Ujerumani, Ubeligiji, Uholanzi, Swideni, Norway, Austria, Uswizi , Malta, Uhispania, Ureno,Ufaransa, Ugririki, Italia, Albania, Yugoslavia, Macedonia, Groatia, Slovenia, Poland, Rumania, Hungary, Bulgaria, Slovakia, Ekistan,Chekislovakia, Lithuania, Estonia, Latvia,Finland,Urusi, Ukraine, Belorusia, Georgia, Armenia, Tajikistan,Uzbekistan, Kazakhstan, Syria, Iraki, Jordan, Lebanon, palestina, Israeli, Yemen, Mashariki ya mbali , Ufilipino, Singapore, Thailand,, Mongolia, Uchina, Cambodia, Japani,Taiwani Korea, Australia, New Zealand, Papua Ginea,(PNG).
Kwa ujumla Masista hawa wapo kwenye mabara 5, nchi 130 duniani, na wananyumba zao 720 duniani,
Je unafahamu Masharti ya kujiunga na shirika la Masista wa Upendo au wa Huruma?
Ili msichana ajiunge na Shirika la Masista wa Upendo hana budi kuwa na sifa zifuatazo;
1).    Binti awe amehitimu kidato cha nne.
2).    Binti awe na cheti kinacholingana na kidato cha nne kinachotambulika na serikali.
3).    Atoke katika familia nzuri ya kikatoliki.
4).    Awe na afya njema ya kimaumbile, kiakili na kiroho.
5).    Awe na umri kuanzia (18-24) katika nchi za Afrika.
6).    Kijana awe na moyo wa umisionari
Tuone changamoto wanazo kumbana nazo:
Kushuka kwa miito, vijana wengi wanapenda kazi za mishahara,baadhi ya wazazi wanapenda kuoza watoto wao na kupata mahari kama vile ng’ombe 100.Changamoto nyingine ni muda mrefu wa malezi  wa miaka minne hivyo wanakata tamaa upesi na kuondoka.
Jumla ya Masista ni, 5,340, wanovisi 60, wapostolanti 50.
Kwa wanaopenda kujiunga na shirika la Masista wa upendo anaweza tuma barua yake kupitia anuani ifuatavyo.
Mkurugenzi wa Miito
Box 858
Tabora.

Na. Thomas Mambo - Tabora



Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU