Posts

Showing posts from November, 2017

SHERIA MPYA YA NDOA: PAPA AWATAKA MAKUHANI KUWA KARIBU ZAIDI NA WANANDOA

Image
Ninayo furaha ya kukutana nanyi wakati wa kuhitimisha kwenu mafunzo kwa wahudumu wa Kanisa na walei, mkutano ulioandaliwa na Mahakama Kuu ya Vatican, ukiwa na kauli mbiu Mchakato mpya wa ndoa na hatua zake kwa ngazi zake za juu ni Mafunzo yaliyofanyika Roma, kama pia mafunzo yanayofanyika katika majimbo mengine.  Mafunzo haya ni ya kupewa sifa na kutiwa moyo ili yaweze kutoa mchango na fursa ya utambuzi katika kubadilishana uzoefu kwa ngazi mbalimbali za Kanisa na umuhimu wa hatua za michakato ya sheria. Ni utangulizi wa hotuba ya Baba Mtakatifu Fransisko Jumamosi 25 Novemba 2017 alipokutana na washiriki wa mafunzo yaliyoandaliwa na Mahakama kuu ya Vatican. Baba Mtakatifu katika  hotuba yake anasema, ni muhimu  kutazama kwa makini Hati mbili za hivi karibuni  zinazohusu “Yesu Kristo Hakimu mwenye huruma” ijulikanayo kama “Mitis Iudex Dominus Iesus” na ile ya “Huruma katika hukumu” maana yake, “Mitis et Misericors Iesus” iliyochapishwa  tarehe 15 Agosti 2015,  na ili

KUELEKEA SINODI YA VIJANA: MASWALI YA VIJANA YAPO MTANDAONI HADI DESEMBA 31

Image
Siku zilizopita kuanzia tarehe 16-17 Novemba 2017 umefanyika mkutano wa tatu wa XIV wa Baraza la kawaida la Sekretarieti Kuu ya Sinodi ya Maaskofu akiwapo hata Baba Mtakatifu Fransisko. Shughuli hiyo ilianza na hotuba ya Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu Kardinali Lorenzo Baldisseri. Katika hotuba yake alianza na salamu kwa Baba Mtakatifu  kwa kumshukuru uwepo wake, zaidi pia kwa tendo la kuhitimisha Sinodi Maalum ya Maaskofu wa  Kanda ya Amazon ambayo itafanyika mwezi Oktoba 2019. Kardinali Baldisseri amewakaribisha washiriki wote wa Mkutano na kutoa taarifa kamili za mchakato wa Sinodi ya XIV   ya Maaskofu  kufikia leo hii, akisisitiza hasa juu ya Hati ya maandalizi na maswali ambayo yametumwa kwa wahusika wote wenye haki, pia juu ya ufunguzi wa mtandao wa moja kwa moja wa maswali kwa vijana, juu ya kuweka mikondo mingine ya kijamii, na juu ya Semina ya Kimataifa iliyokuwa inahusu hali halisi ya vijana, semina iliyofanyika mwezi Septemba mwaka huu. Baada ya hotu

AGIZO LA RAIS MAGUFULI JUU YA HOSPITALI NCHINI LATEKELEZWA

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amekabidhi rasmi Hospitali za Rufaa za Mikoa kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Hatua hiyo imekuja kufuatia pendekezo lililotolewa na Rais John Magufuli Novemba 25 aliyetaka hospitali hizo zitolewe TAMISEMI ziwe chini ya Wizara ya Afya ili kuweza kuwapo kwa mfanano wa sera lakini pia ugawaji wa rasilimali watu katika hospitali hizo. Rais aliyasema hayo alipokuwa akizindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Kampasi ya Mloganzila na kueleza kuwa kumekuwa na utofati mkubwa wa ugawaji wa madaktari katika hospitali za rufaa kutokana na mgawanyo huo kufanywa na wizara mbili tofauti. Mbali na Rais kuagiza hospitali hizo ziwe chini ya Wizara ya Afya ili zisimamiwe vizuri na wataalamu na pia ameiagiza wizara hiyo kurekebisha mgawanyo wa madaktari katika hospitali zote nchini ili ku

MAGAZETINI LEO JUMANNE NOV 28

Image

MAGAZETINI LEO JUMATATU NOV. 27

Image