Posts

Showing posts from September, 2019

Maaskofu wataka mapadri kutoa mahuribi hai si vijembe

Image
Na Padri Anthony Chilumba RAis wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu   Katoliki Mbeya,Mhashamu Gervas Nyaisonga amewataka Wahubiri wa   Neno la Mungu kuzingatia kanuni bora za utoaji mahubiri yao kwenye maadhimisho mbalimbali ya   Liturujia. Ameyasema hayo wakati anafungua Warsha   ya Uboreshaji wa kutoa Homilia iliyofanyika kwenye Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu Katoliki   Tanzania iliyowakutanisha wajumbe wapatao 60 toka majimbo 26, wakiwemo Manaibu wa Maaskofu kutoka majimbo 15. Askofu   Nyaisonga amewaambia washiriki hao kuwa, waamini wanaguswa sana na mahubiri yanayotolewa kanisani,hivyo ingawaje ni ya muda mfupi yanahitajika sana ili kuwatia moyo wakristo wanaoyasikiliza. Kwa mujibu wa Askofu Nyaisonga Ibada mbalimbali zinazoongozwa na mapadri zinapaswa kuwa hai na kwamba uhai huo unachangiwa na mahubiri ya adhimisho husika. “Mahubiri yenu yasidorore wala yasikinaishe wasikilizaji kwa sababu yakiwa hivyo hayatakidhi lengo

Askofu Banzi aadhimisha jubilei miaka 25 ya Uaskofu

Image
  Na Domonic Maro- Tanga. AS kofu wa Jimbo Katoliki Tanga Mhashamu Anthony Banzi ameadhimisha jubilei ya fedha (miaka 25) ya uaskofu. Maadhimisho ya Jubilei hiyo yamefanyika hivi karibuni katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua Chumbageni Jimboni humo. Papa Fransisko amemtumia Salamu za pongezi Askofu Banzi akisema anamshukuru Mungu kwa kulitumikia Kanisa katika Jimbo Katoliki Tanga. Akisoma salamu hizo kwa niaba ya Baba Mtakatu, Balozi wa Baba Mtakatifu Nchini Askofu Mkuu Marek Solczyn’sk amesema kuwa, Papa anampongeza Askofu Banzi kwa utume uliotukuka katika Kanisa la Tanzania na hasa Jimbo la Tanga. Anamuombea baraka za Mungu aendelee kuchunga kondoo wa Mungu na kulikuza Kanisa jimboni Tanga. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC limempongeza Askofu Banzi kwa utume uliotukuka huku likimuombea na kumshukuru kwa kujitoa kwa moyo bila kuchoka kwa muda wa miaka 25 ya uaskofu wake. Akiwakilisha salamu hizo   za TEC Makamu Mwenyekiti wa TEC Askofu Flavian Kassal

Mbunge kuanzisha chama cha Moyo Mtakatifu wa Yesu bungeni

Image
  Rodrick Minja na Ndahani Lugunya, Dodoma MBUNGE wa Rombo, Joseph Selasini amesema ataanzisha tawi la chama cha kitume cha Moyo Mtakatifu wa Yesu katika Jumuiya yake iliyopo Bungeni huku akimwomba Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki   Dodoma, Mhashamu Beatus Kinyaiya kuwa tayari kufanya uzinduzi pindi atakapoanzisha chama hicho cha Kitume. Amesema hayo katika kilele cha Jubilei ya Miaka 100 ya Chama cha Kitume cha   Moyo Mtakatifu wa Yesu kiliyofanyika katika viwanja vya Hija Mbwanga Jimbo Kuu Katoliki Dodoma. Wakati huo huo, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Anna Makinda   ameongoza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Groto ya sanamu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu na kufanikiwa kukusanya TSh 8,493,750. Mbunge Selasini ametoa ahadi hiyo alipopata nafasi ya kuzungumza akiwa miongoni mwa wanachama wapya 75 walipokelewa kwenye Chama cha Kitume cha Moyo Mtakatifu wa Yesu kwenye kilele cha jubilei hiyo. Selasini amemshukuru Spika Staafu Makinda kwa j