Posts

Showing posts from November, 2018

Ask. Chengula azikwa Mbeya

Image
Na Pascal Mwanache, Mbeya W AZIRI wa Fedha na Mipango nchini Dkt. Philip Mpango amesema kuwa ni jukumu la viongozi wa dini kukemea uovu uliopo katika jamii na hata viongozi wa serikali wanaposhindwa kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia watanzania. Ameeleza hayo katika Misa Takatifu ya maziko ya marehemu Askofu Evaristo Chengula wa Jimbo Katoliki Mbeya iliyofanyika kwenye Kanisa la Hija Parokia ya Mwanjelwa, ambapo Dkt. Mpango amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Ponge Magufuli. Dkt. Mpango amesema kuwa marehemu Askofu Chengula alikuwa na uthubutu wa kukemea uovu katika jamii ya Tanzania, jambo ambalo viongozi wa dini hawana budi kuliendeleza. Amebainisha kuwa Askofu Chengula alikuwa ni kiongozi wa mfano kwa waamini wa Mbeya na watu wote. “Waamini wa Jimbo Katoliki la Mbeya na wanachi wa Mbeya Mungu aliwapa zawadi kubwa, aliyoihamisha kutoka Iringa akawaleteeni ninyi. Huyu alikuwa ni kiongozi wa mfano. Aliwaelekeza watu kwa Mungu. Alithamini

Rais Magufuli: Ni wachache wanaoweza kutetea ukweli kama Ask. Chengula

Image
Na Pascal Mwanache, Dar es salaam RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema kuwa ni viongozi wachache wanaoweza kujitokeza hadharani na kusema ukweli kama alivyofanya marehemu Askofu Evaristo Chengula. Amesema hayo katika Misa Takatifu ya kumuombea na kuaga mwili wa Askofu Chengula, iliyofanyika Novemba 26 katika Kikanisa cha Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini jijini Dar es salaam. Akitoa salamu za rambirambi katika misa hiyo Dkt. Magufuli ametoa pole kwa Kanisa kwa kuondokewa na mmoja wa viongozi wa kiroho ambaye daima alithubutu kusema na kusimamia ukweli. “Amemaliza kazi yake salama, ameitangaza Injili na amekuwa mkweli daima. Hakusita kuzungumza ukweli. Hivi karibuni alijitokeza na kupinga vitendo vya ushoga vinavyoshamiri katika jamii yetu. Ni viongozi wachache wanaoweza kujitokeza hadharani na kutangaza ukweli wa Injili” amesema Dkt. Magufuli. Akitoa homilia katika misa hiyo As

Walei ni uhai wa Kanisa-Askofu Ruzoka

Image
Na Thomas Mambo-Tabora A skofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora   Mhashamu Paul Ruzoka amewakumbusha walei kuchukua nafasi yao katika Kanisa bila kusahau wajibu wao wa kutakatifuza malimwengu bila kusita kwani ni wajibu wao. Rai hiyo ameitoa hivi karibuni alipokuwa akitoa mahubiri yake katika kanisa la kiaskofu la Mtakatifu Terezia wa Mtoto Yesu Tabora na kuhimiza waaamini kukimbia dhambi na kuishi maisha yanayompendeza Mungu wakiwa bado hapa duniani. Akitoa mahubiri yake Askofu Mkuu Ruzoka amesema Mtaguso wa Vaticano wa mwaka 1965 ulioweka wazi nafasi ya walei kuwa ni moja ya nguzo muhimu katika uhai wa Kanisa,”Walei ni wengi, wana nguvu na wanapatikana katika kila sehemu kama vile, mitaani, vijijini, vigangoni , maeneo ya kazi, na hata maeneo ya   biashara wakitumika vizuri wana nguvu kubwa ya kueneza Imani Katoliki,” Askofu Mkuu Ruzoka amesema. Aidha amesisitiza umuhimu wa familia zote kuishi Imani Katoliki na kudumisha maadili katika ndoa zao   ili kupata mapadri na