Mapadri msiburuze Misa Takatifu, Ekaristi ndiyo maisha yenu-Ask. Lebulu



Na Sarah Pelaji, Isaack Mwacha -Bagamoyo
Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki  Arusha Mhasham  Josaphat Lebulu amewataka Mapadri kuenzi Ekaristi Takatifu huku akiwaonya wanaokimbiza Misa Takatifu kwa kisingizio cha kujali muda.
Askofu Lebulu ameyasema hayo hivi karibuni katika adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu  ambayo ilikuwa ni maalumu kwa ajili ya Bikira Maria Nyota ya Uinjilishaji Tanzania katika maadhimisho ya miaka 150 ya uinjilishaji Tanzania bara ambayo yalifanyika Bagamoyo ulipo mlango wa Imani.
Ametaka Maadhimisho ya Ekaristi Takatifu yafanywe kwa maandalizi ya kutosha ili yaadhimishwe kwa imani.
“Tuenzi Neno la Mungu, Ekaristi Takatifu na Mama yake. Mimi kama padri nikisahau Injili, nitaleta balaa na kasoro kubwa katika Kanisa, endapo tutamdharau na kumuweka pembeni Mama Maria tutashindwa.
Wajibu wa kwanza wa padri ni kuishi na kuheshimu Neno la Mungu, kuadhimisha Ekaristi Takatifu na kufungamana na Maria Mama wa Kanisa maana huyu Mama ndiye anayetubeba mgongoni na kutufikisha mahali salama,” Amesisitiza Askofu Lebulu.
Aidha amewataka wakristo wote kutambua kuwa urithi pekee wa Uinjilishaji ni Neno la Mungu, Ekaristi Takatifu pamoja na Mama Bikira Maria.
‘Nimekuwa nikijiuliza ni kitu gani kiliwasukuma wamisionari waje kwetu? Ndipo nikafungua maandiko Matakatifu ambayo yalinipa jibu moja,’Nimekuja ili wawe na uzima tena uzima tele.’
Mungu akaniambia kupitia Neno lakwe kwamba, Yesu aliacha zawadi ya neno la Mungu yaani Yeye mwenyewe ambaye ni Neno la Mungu aliyefanyika mwili.
Yesu hakuacha picha yake wala mchoro wake ili wafuasi wake wamkumbuke la hasha aliacha Neno lake na Ekaristi Takatifu ambayo ni mwili wake na alisema twaeni mle, twaeni mnywe.. fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
Alipopokea msalaba wake mama yake alifuata nyuma wakati hakuweza kuelewa lolote lakini alikubuka maneno ya Simeoni ‘Upanga utapenya moyo wako’ alienda mpaka chini ya msalaba  na Yesu alituachia mama yake.
Alimtazama Mwanafunzi aliyempenda akasema ‘Tazama mama yako na Mama tazama mwanao. Mwanafunzi aliyependwa na Yesu  ni mimi na wewe.  Hiyo ni zawadi ya tatu,” ameeelza Askofu Lebulu.
Amesema zawadi hizo Tatu yaani Neno la Mungu, Ekaristi Takatifu na Mama Bikira Maria ndizo zilizowajaa  Wamisionari wakazibeba kila walipotaka kwenda huku wakiongozwa na maneno ya Yesu, ‘Enendeni ulimwenguni mwote… Historia kama tuijuavyo hawa wamisionari waliozikwa hapo kati ya umri wa miaka 20-40 ni Neno la Mungu, Ekaristi Takatifu na Mama Bikira Maria viliwapa nguvu ya kufanya uinjlishaji.
Kuadhimisha Jubilei yetu ya 150 hapa Tanzania tunaona majitoleo ya wamisionari  na waamini watakaposahau chanzo cha majitoleo yao ambayo ni Neno … watakuwa tumekosea mno maana walileta kile kilichoachwa na Kristo wakakieneza kwetu.
“Walipokuja wamisionari  hawakujali kupata taabu maana hata Kristo hakujali kifo maana ni katika kifo tunapata uzima wa milele. Sisi watanzania maneno hayo  yanatuhimiza kuzama kutafuta kiini cha yale Yesu aliyasia katika mioyo ya wamiaionari,”ameeleza.
Ameliasa Kanisa kufanya tathmini ili limshikuru Mungu pale lilipofanikiwa na kuomba kupata mafanikio zaidi lakini pia kukubali pale lilipoanguka ili kuomba toba na kusimama tena.
“Yesu amefanya kazi kupitia wamisionari ni zamu yenu waamini wa Tanzania na anatutahadharisha kuwa yupo mwizi na mawakala zake. Kuna changamoto ya imani  na kuna hatari za waamini wanaochanganya imani,
Kuna kushindwa na kuanguka na tusikose kusema ukweli hapa nimeshindwa na hapa lazima tusimame ila hatutasimama bila kuomba toba.
Tusiangalie kuanguka tu na kukata tamaa bali tupige goti tumwambie Mungu tumekosea atusimamishe maana Mungu anatuambia Moyo uliovunjika na kupondeka hataudharau. Tumwambie Mungu tuhurumie tuweze kuendelea mbele,” amesisitiza.
Ameliasa Kanisa katika kipindi kipya cha uinjilishaji kusia mbegu ya imani kwa watoto na vijana ili wakue katika maisha mfungamano.
“Mwaka 1948 nilifika Kanisani nikafurahishwa na maua nilifikiri ni Mbinguni nikaona masista wa Damu Takatifu na mapadri walivyokuwa wanafanya misa. Nikasikia Neno, waacheni watoto wadogo waonje ukristo na kuanzia hapo nikasema lazima niimbe nikajiingiza kwenye masuala ya imani baadaye nikawa padri.
Sasa msiwache watoto na vijana nyumbani, washirikisheni imani, waende Kanisani, washiriki mafundisho na semina mbalimbali za imani. Ninasisitiza  malezi mfungamano.Watoto waachwe waelekezwe ni marafiki wa Yesu,” amesema.
Aidha ameliasa Kanisa kuwekeza imani kwenye familia kwani  ni jambo la msingi  familia kuwa Kanisa dogo lenye watu wacha Mungu na kuwa kitu kimoja na mapadri, watawa na maaskofu chini chini ya Yesu Kristo na Nyota ya uinjilishaji ambaye ni Mama Maria .
Katika kilele cha maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 150 ya Uinjilishaji nchini Tanzania Novemba 3 mwaka huu Askofu Mkuu Mstaafu Josaphat Lebulu wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha alijumuika pamoja na Askofu Mstaafu Damian Kyaruzi wa Jimbo Katoliki Sumbawanga kumshukuru Mungu kwa miaka 50 tangu walipopewa Daraja Takatifu ya Upadri, huku akisema kama wangekatiswa tamaa katika wito wao tangia wakiwa wadogo wasingelikuwa mapadri na hatimae Maaskofu.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU