Kadinali Pengo asisitiza umuhimu wa Ekaristi Takatifu

Na Philipo Josephat  Kibaha
ASkofu Mkuu wa Jimbo Kuu  Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amefungua rasmi Kanisa dogo la kuabudia Ekaristi Takatifu katika Parokia ya Mt. Fransisko wa Sales Mkuza na kuwataka waamini kutambua umuhimu wa Ekaristi Takatifu katika maisha yao.
Katika uzinduzi wa Kanisa hilo Kardinali Pengo amesema Kanisa hilo la kuabudia Mungu daima linaweza kuonekana dogo katika macho ya waamini lakini licha ya udogo wake ndimo chemchemi ya upendo, huruma ya kimungu ilipo.
Hivyo kila mkristo akitambua umuhimu wa Ekaristi Takatifu maishani mwake atafika kunako kanisa hilo muda wote kusema na Yesu wa Ekaristi.
“Leo tunaiweka parokia yetu katika historia ya Mungu kwa upendo wake kwetu sisi wanadamun na tunafuraha kubwa ya kubariki na kufungua kanisa dogo kwa ajili ya kuabudia Mungu wa daima, hivyo sote tutambue thamani ya Ekaristi Takatifu katikati ya maisha yetu kama alivyosema Baba Mt. Yohana II,” amesema.
Aidha Kardinali Pengo ametumia kuzindua kitabu cha MUNGU NI MUWEZA WA YOTE kilichoandikwa na muumini wa Parokia ya Mkuza Ndugu Mathias Tiyabiyona aliyetembea takribani siku 32 kwa miguu kuelekea Butiama kwenye Kaburi la Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere akiwa na sanamu ya Mama Bikira Maria, na lengo la safari hiyo lilikuwa kumtangaza mama Bikira Maria.
Muamini huyo huyo ameliambia gazeti kiongozi kuwa kabla ya safari hiyo aliyoianza August 4, 2014 hadi Septemba 2, 2014 akiwa kwenye sala ya Rozari Takatifu aliijiwa na sauti masikioni mwake ikimwambia ya kuwa watu wan chi hii ya Tanzania hawajui kuwa mimi ni mwombezi wao, ikiwa ni sauti ya Mama Bikira Maria.
Baada ya uzinduzi huo Kadinali Pengo alielekea kwenye Jubilei ya miaka 50 ya Parokia ya Chalinze. Parokia ya Mt. Fransisko wa Sales Mkuza inaongozwa na paroko Pius Thomas wa Shirika la Mt. Fransisko wa Sales


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU