Rais Magufuli: Ni wachache wanaoweza kutetea ukweli kama Ask. Chengula

Na Pascal Mwanache, Dar es salaam
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema kuwa ni viongozi wachache wanaoweza kujitokeza hadharani na kusema ukweli kama alivyofanya marehemu Askofu Evaristo Chengula.
Amesema hayo katika Misa Takatifu ya kumuombea na kuaga mwili wa Askofu Chengula, iliyofanyika Novemba 26 katika Kikanisa cha Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini jijini Dar es salaam.
Akitoa salamu za rambirambi katika misa hiyo Dkt. Magufuli ametoa pole kwa Kanisa kwa kuondokewa na mmoja wa viongozi wa kiroho ambaye daima alithubutu kusema na kusimamia ukweli.
“Amemaliza kazi yake salama, ameitangaza Injili na amekuwa mkweli daima. Hakusita kuzungumza ukweli. Hivi karibuni alijitokeza na kupinga vitendo vya ushoga vinavyoshamiri katika jamii yetu. Ni viongozi wachache wanaoweza kujitokeza hadharani na kutangaza ukweli wa Injili” amesema Dkt. Magufuli.
Akitoa homilia katika misa hiyo Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Yuda Thadei Ruwaich amesema kuwa kila mbatizwa hana budi kuishi wito wa kumshuhudia Kristo  kiaminifu kwa kila hilo ni jukumu la kila mkristo. Amebainisha kuwa utumishi wa Askofu Chengula ulijaa uaminifu, furaha, ushujaa na uadilifu.
“Hakuogopa kusema ukweli kama ilivyompasa, Mungu alimpa uthubutu katika kuushuhudia ukweli wake. Nasi hatuna budi kuishi kiaminifu wito wetu wa kumshuhudia Kristo, hili ni jukumu la kila mbatizwa, haidhuru ni nani” ameeleza.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU