Posts

Showing posts from February, 2020

CCBRT yazidi kuwatia moyo wenye fistula

Image
LICHA ya uhamasishaji unaofanywa na Shirika   lisilo la Kiserikali linaloshughulika na masuala ya afya la CCBRT,kuwahamasiha   akinamama wenye tatizo la kutoka haja ndogo   au kubwa   bila kujitambua (Fistula)kujitokeza kupata matibabu bure ya ugonjwa huo, idadi inayojitokeza ni ndogo ikilinganishwa na hali halisi. Afisa Uhusiano wa CCBRT   Bw. Abdul Kajumulo ameyasema hayo mwanzoni mwa juma wakati akizungumza na vyombo vya habari vinavyomilikiwa na kusimamiwa na Kanisa Katoliki nchini,mazungumuzo yaliyofanyika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) jijini Dar es Salaam. Amesema   takribani watu 3,000 nchini Tanzania hukabiliwa na ugonjwa wa fistula kila mwaka, lakini kati ya hao ni wagonjwa 1,500 - 2,000 wanafika hospitali kwa ajili ya kupata tiba huku idadi iliyosalia wakiendelea kujificha majumbani, jambo lililoelezewa     kukwamisha juhudi za kupunguza   kasi ya zatizo hilo. Amezitaja   baadhi ya sababu zinazochangia watu kutokupata matibabu kuwa ni pamoja na imani p

Taasisi zatakiwa kuwa na Sera ya Walemavu

Image
    Wenye ulemavu wadai kutengewa makazi ni kuwabagua Na Dalphina Rubyema ILI kujenga   jamii   yenye usawa na kujali makundi   yote, taasisi na mashirika mbalimbali   nchini   yakiwemo ya kidini , yameshauriwa   kutunga Sera   yenye kuwalinda   na kuwatetea watu wenye ulemavu. Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa   Kitengo cha Ujumuishaji wa Watu wenye Ulemavu katika Masuala ya Maendeleo   cha CCBRT, Bw. Frederick Msigala, wakati akizungumza na vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Kuendeshwa na Kanisa Katoliki nchini. Katika mazungumzo   hayo yaliyofanyika katika ofisi za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) zilizopo Kurasini jijini Dar es Salaam, Bw. Msigala amesema licha ya asilimia 9.3 ya Watanzania kutajwa kuwa ni watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali, bado jamii haijalipa umuhimu unaotakiwa kundi hili, jambo linalorudisha nyuma juhudi za serikali na wadau wengine wa maendeleo. Aliyataja baadhi ya mambo yanayokwamisha juhudi hizi kuwa ni pamoja na baadhi ya taasis

Wanaosimamia watoto katika ubatizo wawe waamini waliokomaa kiimani-Ask. Rwoma

Image
Mapadri, wazazi na viongozi wa Kanisa wametakiwa kuwa makini kuwachagua wasimamizi wenye uelewa na Imani, na kuwaonyesha njia wale wote wanaowasimamia   watoto katika Sakramenti mbali mbali za Kanisa Katoliki. Wito huo umetolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba Mhashamu Desderius Rwoma katika homilia yake wakati wa Misa Takatifu ya somo wa Parokia ya Mt. John Bosco katika Parokia ya Mt. Yohani Bosco - Kamishango Jimboni humo. Katika homilia yake Askofu Rwoma amesema kuwa, ni vizuri wazazi wakawachagulia watoto wao wasimamizi wenye sifa na waliokomaa kiimani katika Sakramenti za ubatizo na kipaimara. ''Katika Sakramenti za Kanisa kuna mtu anaitwa msimamizi, sasa sifa kuu ya msimamizi ni kumuonyesha njia yule unayemsimamia, mzazi anapaswa kuwa kiongozi kwa yule unaye msimamia na kiasi cha maisha anayoishi unaweza kusema huyu anaweza kuwa mtu mwema sio kuokota okota tu mtaani. Aidha, anayekuwa msimamizi lazima amjue vyema anayemsimamia ili  kumshauri asije akapotea