Taasisi zatakiwa kuwa na Sera ya Walemavu

   
Wenye ulemavu wadai kutengewa makazi ni kuwabagua

Na Dalphina Rubyema

ILI kujenga  jamii  yenye usawa na kujali makundi  yote, taasisi na mashirika mbalimbali  nchini  yakiwemo ya kidini , yameshauriwa  kutunga Sera  yenye kuwalinda  na kuwatetea watu wenye ulemavu.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa  Kitengo cha Ujumuishaji wa Watu wenye Ulemavu katika Masuala ya Maendeleo  cha CCBRT, Bw. Frederick Msigala, wakati akizungumza na vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Kuendeshwa na Kanisa Katoliki nchini.
Katika mazungumzo  hayo yaliyofanyika katika ofisi za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) zilizopo Kurasini jijini Dar es Salaam, Bw. Msigala amesema licha ya asilimia 9.3 ya Watanzania kutajwa kuwa ni watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali, bado jamii haijalipa umuhimu unaotakiwa kundi hili, jambo linalorudisha nyuma juhudi za serikali na wadau wengine wa maendeleo.
Aliyataja baadhi ya mambo yanayokwamisha juhudi hizi kuwa ni pamoja na baadhi ya taasisi na mashirika mbalimbali  nchini kutokuwa na Sera ya Walemavu jambo  ambalo amesema linawanyima stahiki zao.
“Ni kutokuwa na Sera ya Walemavu ndiko kunakosababisha hata miundombinu ya  baadhi ya taasisi kutokuzingatia mahitaji  ya walemavu.
Unakuta taasisi  ina kumbi nzuri za mikutano lakini ujenzi wake ni wa ghorofa na hakuna lifti kwa ajili ya watu wenye ulemevu… vivyo hivyo mazingira unakuta yana barabara zenye ngazi ,lakini hakuna ngazi mbetuko maalum kwa kundi hili. Hata sehemu za kujisitiri si rafiki kwa walemavu,” amesema.
Hata hivyo amesisitiza kuwa, Sera hiyo ilinde makundi yote ya walemavu wakiwemo wale  wa viongo, kutokuona, ngozi,  viziwi na wale wenye upoozi wa ubongo.
Bw.Msigala ambaye ni mlemavu wa viungo amesema, kutokulijali kundi  la walemavu ndiko kunakosababisha kundi hili kuendelea kunyanyapaliwa huku baadhi ya watu wakiwachukulia kama  watu wanaohitaji hisani  jambo ambalo siyo sahihi.
“Ulemavu si dhambi wala laana! Si kundi linalotakiwa kutengwa na jamii, badala yake tunatakiwa kuwawezesha kwa kuangalia mahitaji yao ya msingi ikiwemo elimu na miundombinu rafiki ya kupata elimu hii..
Tunauwezo  wa kupambanua mambo kama ilivyo kwa binadamu wengine wasiyo walemavu , tatizo ni kwamba hatupewi kipaumbele…hatupelekwi shule badala yaketunafichwa majumbani, na hili linachangia sana idadi ya watu wenye ulemavu wasiyojua kusoma na kuandika kuwa kubwa ikilinganishwa na wale watu wa kawaida,” amesema.

Kitakwimu alisema kwamba, asilimia 45 ya Watu wenye ulemavu nchini Tanzania,hawajui kusoma na kuandika na katika watoto 10 wenye ulemavu, wanne kati yao hawaendi shule na chini ya asilimia tano ndiyo walioajiriwa katika  sekta rasmi.
“Tusichukuliwe kama watu wakupewa hisani… sisi ni binadamu kamili. Tuna akili na uwezo wa kupembua mambo hata darasani tunafanya  vizuri…mfano ni kwangu mimi ambaye wazazi wangu hawakuniona mzigo tangu awali, walinisomesha.
 “Sekondari nilisoma Tosamaganga  Iringa, Digrii yangu ya kwanza nilisoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Masters nimesoma Uingereza… ninauwezo ndiyo maana hata CCBRT wameniajiri na ajira yangu siyo ya upendeleo ni stahiki yangu, hivyo tusiwadharau watu wenye ulemavu bali tuwawezeshe kulingana na mahitaji  yao,” amesisitiza.
Amesema kuwawezesha huku  kusiwe kule kwa  kuwajengea nyumba au kuwatengea makazi maalum, badala yake wapewe elimu, wawezeshwe  kupata taarifa kila kundi kulingana na mahitaji yake ikiwa ni pamoja na kuwekewa wataalam wa alama, maandishi kuwa katika mfumo wa nukta nundu  na mahitaji mengineyo.
“Kutujengea nyumba au kututafutia makazi maalum ni zaidi ya kututenga sisi watu wenye ulemavu … ni sawa na kutuambia tujitenge na jamii tuishi peke yetu …inasahau  kwamba tunayo haki ya kuishi na ndugu,jamaa na familia zetu kwa ujumla…hili nalo liangaliwe kwa  mapana linatuumiza,” amesisitiza Bw.Msigala.
Amesema yote haya yataondoka endapo serikali, wadau na jamii kwa ujumla itatengeneza mazingira rafiki ya kuwawezesha watu hawa wenye ulemavu.



Comments

  1. If you're trying hard to lose kilograms then you absolutely have to get on this brand new custom keto meal plan.

    To create this keto diet service, licensed nutritionists, fitness trainers, and cooks have joined together to develop keto meal plans that are useful, convenient, economically-efficient, and fun.

    From their first launch in January 2019, hundreds of clients have already remodeled their body and health with the benefits a great keto meal plan can provide.

    Speaking of benefits: clicking this link, you'll discover 8 scientifically-certified ones given by the keto meal plan.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU