Posts

Showing posts from August, 2017

MKUTANO MKUU WA 17 WA SHIRIKISHO LA MASISTA WAKATOLIKI NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI (ACWECA).

Image
Na Pascal Mwanache Mkutano huo umefunguliwa Agosti 26, 2017 kwa Misa Takatifu iliyoongozwa na Rais wa Baraza la Kipapa la Maisha ya waliowekwa wakfu Mwadhama Joao Kardinali Braz de Aviz kutoka Vatikani. Katika Misa Takatifu ya ufunguzi wa mkutano huo Kardinali Joao amewaasa watawa wanaounda shirikisho hilo kutomezwa na tama ya fedha katika utume wao na badala yake wajikite katika kutoa huduma bila kutegemeamalipo ya hapa duniani. Mkutano huo wa unatarajiwa kufanyika hadi Septemba 2, 2017 katika kituo cha mikutano cha Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini jijini Dar es salaam. Umoja huo unaundwa na nchi 9 ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Malawi, Zambia, Ethiopia, Sudani ya Kusini, Sudani na Eritrea. Baadhi ya wageni waliohudhuria ufunguzi wa mkutano huo ni pamoja na Askofu wa Jimbo Katoliki Bunda Mhashamu Renatus Nkwande, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Eusebius Nzigilwa, na Balozi wa Papa nchini Askofu Mkuu

Kanisa halitadhoofishwa-Ask Ndimbo

Image
n   Na Pascal Mwanache ASKOFU wa Jimbo Katoliki Mbinga na Mwenyekiti wa Huduma za Jamii kwa upande wa Elimu, katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Mhashamu John Ndimbo amesema kuwa, licha ya vikwazo na changamoto wanazokutana nazo katika jitihada za kumkomboa mtanzania dhidi ya ujinga, Kanisa Katoliki halitarudi nyuma wala kudhoofishwa kwa kuwa utoaji wa elimu ni sehemu ya kazi ya uinjilishaji ya Kanisa. Ameeleza hayo hivi karibuni wakati akifungua Mkutano wa Mwaka wa Makatibu wa Elimu kutoka Majimbo Katoliki Tanzania, uliofanyika TEC Kurasini jijini Dar es salaam. Askofu Ndimbo amesema kuwa siku zote uwepo wa Kanisa Katoliki unatambulishwa kwa uwepo wa huduma za kijamii na kusema kuwa hakuna uinjilishaji pasipo makuzi ya kitaaluma. “Elimu ndiyo inayomfanya mwanadamu kwanza ayajue mazingira yake, ajitambue yeye ni nani na kisha imfahamishe uhusiano wake na Mungu. Miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara inapata maana zaidi kwa jinsi sekta ya elimu ilivyokua kati

Mvimwa wapata Abate Mpya

Image
n   Na Emanuel Mayunga Sumbawanga WA TAWA wa shirikala Mtakatifu Bernediko wa Abasia ya Roho Mtakatifu Mvimwa   WAMEPATA Abate mpya Padri Pambo Martin Mkorwe OSB. Akiongoza Ibaada ya Misa Takatifu   kumuombea   Abate Pambo   Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga   Mhashamu Damian Kyaruzi amemuasa Abate Pambo kufuata mfano wa Mt. Pio wa X Papa, anayekumbukwa August 21 ambaye alijitoa kulihudumia Kanisa la Mungu bila kujibakiza. Akiwashukuru wananchi na waamini wa jimbo la Sumbawanga abate Pambo OSB   amemshukuru askofu na waamini kwa mapokezi na kumuombea na kuahidi kufanya kazi kwa moyo kadiri ya matakwa ya Mama Kanisa. Abate Pambo atasimikwa August 26 mwaka huu katika Makao Makuu ya Shirika Mvimwa Parokiani Kate jimboni Sumbawanga . Aidha Abate huyo amesema anaongozwa na kauli mbiu   DUC IN ALCUM (Tweka mpaka kilindini) Historia   fupi Abate Pambo Martin-Angelica Mkorwe OSB Abate Pambo Martin-Angelica Mkorwe alizaliwa tarehe 15/08/1975 huko Uwemba Mission, kat

Kard.Pengo aikabidhi serikali mradi wa kisima

Image
n   Na Pascal Mwanache, Dodoma KANISA Katoliki Jimbo Kuu la Dar es salaam limekabidhi mradi wa kisima kwa serikali, katika kituo cha mafunzo kwa watoto (mahabusu ya watoto) cha Upanga jijini Dar es salaam, huku serikali ikiazimia kujifunza kupitia jitihada za Kanisa katika kujenga jamii ya watanzania yenye maadili, upendo na kujali wengine. Akikabidhi mradi huo kwa niaba ya watoto wa Shirika la Kimisionari la Utoto Mtakatifu, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amesema kuwa Kanisa linajikita katika utoaji wa huduma za kijamii kuonyesha kuwa linaunga mkono jitihada za serikali katika kuandaa taifa adilifu linaloongozwa na upendo bila kujali tofauti za uchumi, siasa au dini, kwa manufaa ya watanzania wote. “Watoto ndiyo tumaini la kila taifa. Kadiri tunavyokuwa na watoto wenye maadili, wale wanaojua kipi kifanywe ili kujenga taifa, tunaweza kuwa na matumaini kwa taifa la kesho. Kuonyesha kwamba Kanisa hatuko mbali na serikali ye