Posts

Showing posts from October, 2019

Jubilei miaka 75 Masista wa Upendo

Image
‘Mkiushinda ubinafsi mtafanikiwa’ Na Pascal Mwanache, Mbingu MASISTA wa Shirika la Upendo wa Mt. Fransisko Mahenge wameaswa kufanya kazi kwa kushirikiana huku wakiweka kando ubinafsi ili kazi zao ziendelee kumtukuza Mungu. Hayo yameelezwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Tundu-Masasi Mhashamu Filbert Mhasi katika Misa Takatifu ya kuwakumbuka marehemu waanzilishi wa shirika hilo la masista pamoja na masista waliofariki, ikiwa ni sehemu ya sherehe ya jubilei ya miaka 75 ya shirika la masista wa upendo wa Mt. Fransisko Mahenge. Akitoa homilia katika misa hiyo Askofu Mhasi amewaasa masista hao kutotafuta mtetezi mwingine zaidi ya Mungu pale wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali katika utume wao, bali wadumu katika uthabiti wa imani yao na Mungu atawatetea. “Inatupasa kumshukuru Mungu kwa imani tuliyojaliwa kupitia Kristo. Waanzilishi wa shirika hili walipigana vita vizuri na waliamini kuwa kuna maisha baada ya kifo. Ndiyo maana wakawa imara katika imani yao. Hawakuwa wabinaf

Msitumie vibaya utajiri wenu -Askofu Kinyaiya asema

Image
Na Ndahani Lugunya na Rodrick Minja, Dodoma Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya, amekemea tabia ya baadhi ya wakristo waliopewa utajiri na Mwenyezi Mungu kuutumia vibaya utajiri huo hususani kwa kuwanyanyasa wanyonge, yatima, masikini na wasiojiweza. Ameyasema hayo wakati akitoa homilia yake kwenye adhimisho la sadaka ya Misa Takatifu, katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Damu Azizi ya Yesu-Kisasa Jimboni Dodoma, Misa iliyokwenda sambamba na utoaji wa sakramenti Takatifu ya kipaimara kwa vijana 76 wa Parokia hiyo. Katika homilia yake Askofu Kinyaiya amesema kuna baadhi ya wakristo wamejaliwa kupata utajiri kwa halali kabisa, lakini kosa linakuja pale mtu anapoutumia utajiri huo kwa ubadhilifu na kuzitumia katika matumizi yake ya kila siku pasi na mpangilio mzuri. “Mmejaliwa utajiri na Mwenyezi Mungu hivyo utumieni kwa kutenda mema na sio kunyanyasa wengine ambao hawakujaliwa utajiri huo kwani hata ipo siku mwenyezi

‘Tumieni mali zenu kuwasaidia masikini’

Image
Jimmy Mahundi, Mtwara W aamini   wametakiwa kutumia mali,utajiri na karama mbalimbali walizojaliwa na Mungu kuutafuta ufalme wa Mungu kwa kuwasaidia wahitaji   badala ya kuzitumia kwa maslahi binafsi. Hayo yamesemwa hivi karibuni na Abate wa Abasia ya Ndanda Prasidus Mtunguja OSB,wakati wa homilia ya jumapili ya 26 ya mwaka c wa Kanisa iliyofanyika katika Kanisa la Watakatifu Petro na Paulo jimboni Mtwara. Ameitaka jamii ya waamini kutumia mali zao kwa kuwakumbuka wahitaji na maskini katika maeneo yanayowazunguka. Abate Mtunguja amesema kuwa   Mungu amewajalia watu mbalimbali vipawa na mali ambazo wengi wanatumia wao pekee pasipo kuwaangalia wenye shida katika maeneo yao. Hali hiyo inasababisha maskini kuendelea kuteseka na kukosa huduma msingi za binadamu. nafasi na kwa kufanya hivyo mali haiwasaidii kuuikia ufalme wa mbingu. “Ni muhimu na wajibu kwa kila mmoja kuwasaidia katika mahitaji yao ikiwa ni pamoja na ushauri,elimu na vitu mbalimbali.Hiyo ni njia mojawapo wa