Metropolitani ya Tabora yazindua Kongamano la Ekaristi Takatifu

Askofu Mkuu Paul Ruzoka wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora akiwa ndani ya kanisa Kuu la Mtakatifu Terezia wa Mtoto Yesu Yesu Tabora.
Na. Thomas Mambo -Tabora.
Majimbo yanayounda Kanda ya Magharibi (Metropolitani ya Tabora) hivi karibuni imefanya uzinduzi wa Kongamano la Ekaristi Takatikafu katika Makao Makuu ya Kandahiyo  katika Jimbo Kuu Katoliki Tabora ikiongozwa na kauli mbiu “Ekaristi Takatifu , Chemchemi ya Uzima Wetu.”
Misa hiyo ya uzinduzi iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mhashamu  Paul Ruzoka imefanyika hivi karibuni  katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Terezia wa Mtoto Yesu jimboni Tabora.
Askofu Ruzoka amesisitiza umuhimu wa kutumia mali na majaliwa ambayo Mungu anampatia kila mmoja  ili yamsaidie katika maisha yake ya hapa duniani na baadaye katika uzima wa milele.
Aidha amesema kuwa katika ulimwengu wa sasa mwanadamu anaweza kutekwa nyara na mali za dunia hii akasahau kuona na kujali shida ya jirani yake.
“Kupata mali ni jambo nzuri na halina shida yoyote kwa mwanadamu bali zitumike kwa maandeleo ya mwanadamu kiroho na kimwili.
Ni  vyema kujiwekea hazina  mbinguni ili baada ya maisha haya zitufae pia katika maisha baada ya kifo.
Kila mmoja wetu aone kuwa  katika kila mwanadamu kuna sura ya Mungu. Kwamba kila unalofanya unamfanyia Kristo mwenyewe.
 Tunaweza kusoma haya yote katika Injili ya Mathayo 25:31-46, tukifanya hayo yote basi tunakuwa tumeanza safari ya kwenda mbinguni, safari ambayo tunapaswa kuifanya kila siku kila mmoja wetu kwa kadri ya wito wake,” amesema.
Katika Adhimisho hilo la Misa Takatifu ya ufunguzi wa Kongamano hilo, Askofu Ruzoka amesema Kongamano la kwanza lilifanyika huko Ufaransa na Kongamano lijalo la mwaka 2020 katika Jimbo Kuu Katoliki Tabora litakuwa la 52.
Katika Tanzania, Kongamano lijalo litakuwa Kongamano la nne baada ya lile lililofanyika  Dodoma, Iringa na Mwanza .
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wajumbe kutoka Jimbo Katoliki  Kigoma, Jimbo Katoliki Mpanda, Jimbo Katoliki Kahama , Jimbo Kuu Katoliki Tabora na Jimbo Katoliki Singida.
Aidha Askofu  Ruzoka amesema makongamano haya ni fursa ni shule ya kujitathmini wapi pamelegea ili paimarishwe na wapi pako vizuri basi padumishwe zaidi.

 Kilele cha Kongamano la Ekaristi Takatifu kinatarajiwa kuwa mwakani(2020) kuanzia Julai 1-5 mwaka 2020 katika Jimbo Kuu Katoliki Tabora na litahudhuriwa na wa kristo kutoka majimbo yote katoliki ndani ya Tanzania na baadhi ya wageni kutoka nje ya Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU