‘Tumieni mali zenu kuwasaidia masikini’

Jimmy Mahundi, Mtwara
Waamini  wametakiwa kutumia mali,utajiri na karama mbalimbali walizojaliwa na Mungu kuutafuta ufalme wa Mungu kwa kuwasaidia wahitaji  badala ya kuzitumia kwa maslahi binafsi.
Hayo yamesemwa hivi karibuni na Abate wa Abasia ya Ndanda Prasidus Mtunguja OSB,wakati wa homilia ya jumapili ya 26 ya mwaka c wa Kanisa iliyofanyika katika Kanisa la Watakatifu Petro na Paulo jimboni Mtwara.
Ameitaka jamii ya waamini kutumia mali zao kwa kuwakumbuka wahitaji na maskini katika maeneo yanayowazunguka.
Abate Mtunguja amesema kuwa  Mungu amewajalia watu mbalimbali vipawa na mali ambazo wengi wanatumia wao pekee pasipo kuwaangalia wenye shida katika maeneo yao.
Hali hiyo inasababisha maskini kuendelea kuteseka na kukosa huduma msingi za binadamu.
nafasi na kwa kufanya hivyo mali haiwasaidii kuuikia ufalme wa mbingu.
“Ni muhimu na wajibu kwa kila mmoja kuwasaidia katika mahitaji yao ikiwa ni pamoja na ushauri,elimu na vitu mbalimbali.Hiyo ni njia mojawapo wa kujitafutia Ufalme wa Mungu,” amesema.
Aidha amedai kuwa, kuwa na mali au fedha sio tatizo, bali ni kuona vitu mtu alivyojaliwa na  Mungu anavitumiaje katika kujiwekea akiba ya kweli Mbinguni.
Pia amebainisha lipo tatizo kubwa na sugu kwa watu wengi katika jamii ya sasa kuwa na tabia ya uchoyo na kukosa huruma ka wahitaji na wenye shida,amesema hali hii ni hatari sana na kwa kufanya hivyo ni kukosa shukrani kwa Mungu.

Hata hivyo amesema kuwa, matajiri wengi hawalaumiwi kwa kwa kuwa na mali bali uchoyo wao wa kuangalia wahitaji bila kujua kuwa, kusaidia wahitaji ni kuiishi Injili na huo ndio uinjilishaji wa kweli.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU