Wakristo wasilisome neno la Mungu kwa mazoea- Padri asisitiza


Waamini wametakiwa kulisoma, kulisikiliza na kuliishi Neno la Mungu linaloongoza Maisha ya kila mwanadamu.
Hayo yamesemwa huvi karibuni na Priori Msimamizi wa Abasia ya Peramiho Padri Silvanus Kassy OSB,  wakati akihubiri katika misa ya maziko ya sista Miriam Mbawala OSB, iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Agenes Chipole Jimbo Kuu Katoliki Songea.
Padri Kessy amesema kuwa, waamini waache tabia ya kulisoma na kulisikiliza Neno la Mungu, kwa mazoea bali walitafakari na kulielewa ili lilete mabadiliko katika maisha ya kila mmoja wetu.
Aidha amesema neno la Mungu linapotuambia tubuni na kiamini Injili, linatutaka kila mtu binafsi kutubu, kufanya toba na kuiamini Injili na kuamini kabisa uwepo wa Mungu na neno lake.
Amefafanua kuwa, neno la Mungu linatuambia tupendane, tuheshimiane, tusaidiane,tusameheane, tutiane moyo na kufarijiana katika matatizo, hivyo linatudai kulifanyia kazi katika maisha na neno hilo lilete mabadiliko katika kila Nyanja ya maisha.
Padre Kessy amesema kuwa, tunapofanya maziko ya sista Miriam tunadaiwa kuliishi neno la Mungu na kuwa na Imani na Mungu.
 Amesema sisi sote ni wapita njia katika dunia hii na kwamba hatutaweza kamwe kumwendea Mungu pasipo kupitia kifo, kwani hata Bwana wetu Yesu Kristu kabla ya kuingia katika utukufu alionja mauti.
Hivyo amewataka kujiandaa kikipokea kifo na sio kikikimbia.
“ Baadhi yetu tumekuwa tunakikimbia kifo wakati mwingine kwa kutumia hata njia haramu ili tusife kama kwenda kupata mazindiko, kwenda kwa waganga ili watugange. Hayo hayasaidii,” amesema.
Aidha amesema neno la Mungu linasisitiza daima waamini wakeshe kwa sababu hatujui siku wala saa ya kifo chetu.
Akizungumzia wasifu wa sista Miriam  aliyefariki akiwa na umri wa miaka 94 ya kuzaliwa na miaka 71 ya maisha ya nadhiri za kitawa Padri Kessy amesema sista Miriam alikuwa mtu aliyeishi kadiri ya wito wake wa utawa, alikuwa thabiti katika wito wake, mwenye mapendo kwa Mungu na jumuiya yake,na mwenye mapendo ya pekee kwa watoto.
 Pia sista Miriam alikuwa mtu mwenye huruma, mkarimu, mvumilivu, mwenye bidii katika utume wake na mtu wa sala.
Akitoa neno la shukrani mama mkuu wa shirika la masista Wabenediktini wa Mtakatifu Agens Chipole Sista Maria Asante Goliama OSB, amesema, anawashukuru viongozi wote wa Kanisa kwa masakramenti na malezi yaliyofanikisha sista Miriam kuwa mtawa aliyeishi kifadhila.
Sista Asante amewashukuru pia masista wa Tutzing Peramiho waliokuwa walezi wa kwanza wa shirika la Mtakatifu Agens Chipole hadi lilipoweza kujiongoza lenyewe.
Amesema marehemu sista Miriam ni kati ya masista wa kwanza walioanzia maisha yao Peramiho na kuja kuanzisha makao mapya Chipole ambapo hadi sasa wamebaki masista watatu tu waliotoka Peramiho.


Comments

  1. Water Hack Burns 2 lb of Fat OVERNIGHT

    More than 160 000 women and men are hacking their diet with a easy and secret "liquid hack" to drop 2 lbs every night as they sleep.

    It is very simple and works with everybody.

    You can do it yourself by following these easy steps:

    1) Go get a clear glass and fill it up half glass

    2) Then follow this crazy HACK

    and you'll be 2 lbs lighter the next day!

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU